Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Bw.Matina Nkurlu kushoto akifuatilia kwa umakini jinsi Afisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude, anavyomuelekeza Bw. Mweusi Mohamed Mweusi, namna ya kifaa cha kuchajia simu kwa kutumia umeme wa Jua (Readset Solar Charger)kinavyounganishwa na kuanza kufanya kazi leo Katika banda la kampuni ya Vodacom lililoko katika maonesho ya Wiki ya Huduma za kifedha na uwekezaji yanayofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa maofisa wa Vodacom akitoa maelezo kwa baadhi ya wajasiriamali wanaopata mafunzo katika maonesho ya Wiki ya Huduma za kifedha na uwekezaji yanayofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam, Kampuni ya Vodacom imetoa mafunzo kwa wajasiriamali hao ya namna ya kujiunga na kunufaika na fursa ya mikopo isiyokuwa na riba inayotolewa kwa wanawake wajasiriamali wadogowadogo MWEI.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: