Lydia Sakaya akisimama pamoja na waalimu wa shule za msingi Themi na Uhuru za Arusha baada ya kukabishiwa vibao vyakuandikia.
 Watoto wakibeba vibao waliopewa na kampuni ya Tigo wakati wa ghafla yakugawa jana Arusha.
 Lydia akiwakabidhi vibao vyakuandikia kwa waalimu bw. Zebedario Mollel wa shule ya msingi wa Themi na Bi. Eusebio Matamwa mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi ya Uhuru.

 Mwalimu wa shule za msingi Themi na Uhuru za Arusha akijaribu kuandika katika ubao waliokabidhiwa. 

Tigo imekabidhi vibao vya shule elfu mbili kwa shule mbili jijini Arusha. Msaada huu imefuatiliwa na msaada ya kibinafsi ya vibao vyakuandikia kwa niaba ya Christina na Max Stenbeck, ambayo ni wadau wakubwa wa kampuni ya Millicom International Cellular (MIC), kampuni ya Tigo Tanzania. 

Vibao vya kuandikia zilikabidhiwa kwenye shule za msingi kuwasaidia waalimu ambao wanahitaji vibao hivi kuboresha elimu mikoani. Kama ongezeko, waalimu hawa wataweza kutumia hizi vibao katika eneo mbali mbali, hata nje ya darasa, wakiongeza hamu yakuendelea kusoma na kuanzisha aina nyingine ya kujifunza. Vibao hivi ambayo unaweza kutumia mahali popote inaendana vizuri na ukabidhi wa vibao hivyo ambayo vinaitwa ‘lapdesk’. 

“Ni sahihi kwa Tigo, kampuni ambayo inatoa huduma popote nchini kwa wateja wake, kusaidia elimu ya waTanzania kwa aina mpya” Christina Stenbeck alisema wakati akifanyiwa mahojiano kwa simu katikati ya ziara yake ya nchi mbalimbali ambapo Tigo ina ofisi ndani ya Africa na Amerika ya kusini.   

Kwakutoa msaada huu, Tigo inaendelea kuwekeza kwenye elimu ya Tanzania. Hii pia itasaidia waalimu ambayo wanafanya kazi kwenye mazingira magumu shuleni.

Tigo inaendelea kuunga mkono elimu kwa kugawa vibao aina ya lapdesks ambayo zinatumiwa kusaidia watoto kwa ambayo vinawasaidia wanafunzi kuweza kujifunza michoro ya maumbo mbalimbali kama vile alfabeti, tebo ya kuzidisha na aina mbalimbali za rangi ikikabidhiwa na Tigo na ikisaidia kuboresha elimu ya Tanzania. Tigo inaendelea kugawa hizi vibao ikiwa mpango wao yakusaidia elimu.  

Akiongea Arusha jana wakati wakutoa msaada huu, mwakilishi wa Tigo, Bi Lydia alisema kwamba anategemea kwamba hizi vibao vitasaidia watoto na wataweza kujifunza zaidi hata kama hawapo shuleni. 

Sisi kama kampuni ya Tigo, tunalazimika kutoa mchango katika elimu ya watoto na, kwa sababu hii, tuliamua kuvigawa hizi vibao, pamoja na msaada yaki binafsi iliyotolewa na Stenback “ alisema 
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: