


Dodoma.
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeingilia kati mgogoro wa matumizi ya ardhi unaomhusisha mwekezaji Rashid Kwanzibwa katika eneo la Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro, mkoani Geita, kufuatia madai ya kubomoa baadhi ya majengo yaliyopo kwenye maeneo ya serikali na kuanzisha miradi bila kufuata taratibu.
Akizungumza leo Januari 26, 2026 jijini Dodoma, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amesema Wizara yake kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI imeanza kushughulikia suala hilo kwa kina ili kuhakikisha mgogoro huo unapatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa mujibu wa sheria na taratibu za matumizi bora ya ardhi.
Dkt. Akwilapo amewakumbusha wamiliki wote wa ardhi nchini kuzingatia matumizi yaliyobainishwa katika hati miliki zao, akisisitiza kuwa mmiliki yeyote anayepanga kubadili matumizi ya eneo lake anatakiwa kuomba na kupata kibali cha mabadiliko ya matumizi kama sheria inavyoelekeza.
“Hatua hii itasaidia kuhakikisha maeneo yanaendelezwa kwa mpango, kupunguza migongano ya matumizi ya ardhi, kulinda mazingira na kuhakikisha miji yetu inakuwa nadhifu,” amesema Waziri.
Ameongeza kuwa uendelezaji wowote wa ardhi unapaswa kuzingatia sheria za mipango miji na vijiji, ikiwa ni pamoja na kupata vibali kutoka mamlaka husika kabla ya kuanza utekelezaji wa mradi wowote.
Kwa mujibu wa Waziri, timu ya wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi na TAMISEMI tayari ipo kazini kuchunguza kwa kina sakata hilo, na baada ya uchunguzi kukamilika, Serikali itatoa taarifa rasmi ya pamoja kueleza hatua zilizofikiwa.
Hatua ya Wizara kuingilia kati imekuja baada ya kusambaa kwa picha na taarifa katika mitandao ya kijamii zikionesha Kamati ya Fedha na Uchumi ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita ikisitisha shughuli za ujenzi wa vibanda vya maduka katika eneo la viwanja vya CCM Katoro, kufuatia madai kuwa mwekezaji aliingia katika maeneo ya serikali ya kijiji yaliyopo Kitongoji cha Katoro Center.
Serikali imesisitiza itaendelea kusimamia matumizi sahihi ya ardhi nchini ili kulinda maslahi ya umma, kudumisha amani na kuhimiza maendeleo endelevu katika maeneo yote.
Wananchi waliohudhuria uzinduzi huo wameeleza kufurahishwa na mpango huo, wakisema utasaidia kupunguza migogoro ya ardhi, mirathi, ndoa na masuala mengine ya kisheria ambayo yamekuwa yakisumbua jamii kwa muda mrefu.Mpango wa uanzishwaji wa kamati za ushauri wa kisheria na kliniki za sheria Manyara unatarajiwa kuwa chachu ya kuimarisha utawala wa sheria, kuongeza uelewa wa haki za msingi na kujenga jamii yenye haki na usawa zaidi.


Buhigwe. Tarehe 27 Agosti 2025: Akizindua tawi la Benki ya CRDB wilayani Buhigwe pamoja na kupokea madarasa mawili ya shule ya sekondari, Makamu wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango ameisifu Benki ya CRDB kwa jitihada zake za kutanua huduma jambo linalosaidia kuongeza ujumuishaji wa kiuchumi kwa wananchi.
“Benki ya CRDB mmekuwa mnatoa hatifungani ikiwamo hii ya sasa hivi mnayoendelea kuiuza ya CRDB Al Barakah Sukuk lakini ni watu wachache sana wanaelewa maana ya hatifungani na namna wanavyoweza kunufaika nazo. Nawasihi mtoe elimu ya huduma zote mlizonazo pamoja na fursa za uwekezaji mnazozileta kwa wananchi,” amesema Mheshimiwa Dkt. Mpango.
“Mpaka Juni 2025, Benki yetu ilikuwa imepokea amana za wateja kiasi cha shilingi trilioni 14 na kukopesha jumla ya shilingi trilioni 12.25. Katika kipindi cha miaka 30 cha uwepo wa Benki yetu ya CRDB, tumekua na kutanua mtandao wetu wa huduma kutoka matawi 19 yaliyokuwepo mpaka zaidi ya 260 tukilijumuisha hili tunalolizindua leo.
Akizungumzia kuhusu uwekezaji kwa jamii, Nsekela amesema Benki ya CRDB hutenga asilimia moja ya faida yake baada ya kodi kila mwaka ili kuwekeza kwenye miradi ya wananchi hasa iliyopo kwenye sekta ya elimu, mazingira, afya na uwezeshaji wa wanawake na vijana.
Licha ya msaada huo uliotolewa kwa Shule ya Sekondari kibande, Benki ya CRDB ilishapeleka madawati 40 yenye thamani ya shilingi milioni 3.35 kwa Shule Msingi Kasebuzi iliyopo wilayani Kibondo, madawati 50 yenye thamani ya shilingi milioni 3.75 kwa Shule Msingi Ruyenzi ya Kakonko, madawati 40 yenye thamani ya shilingi milioni 3.4 kwa Shule ya Nguruka ya Uvinza, na madawati 40 yenye thamani ya shilingi milioni 3.075 kwa Shule Msingi Sokoine ya Kigoma Vijijini pamoja na madawati 40 yenye thamani ya shilingi milioni 4 Shule Msingi Kabulazili ya Kasulu Mjini.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wakwanza kushoto) akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa makazi ya watumishi wa umma Kijiji cha Kijiweni, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi mkoani Lindi

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (aliyevaa miwani) akisisitiza jambo kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kijiweni, Bw. Hassan Kalembo (wapili kutoka kulia) na Mwalimu wa Taaluma wa Shule hiyo, Bw. Samson Bihole mara baada ya Katibu Mkuu huyo kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa makazi ya watumishi wa umma katika Kijiji cha Kijiweni, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi mkoani Lindi.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (kushoto) akitoka kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa makazi ya watumishi wa umma katika Kijiji cha Kijiweni, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi mkoani Lindi. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kijiweni, Bw. Hassan Kalembo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (watano kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi kutoka katika ofisi yake na Viongozi na Watendaji wa Shule ya msingi Kijiweni mara baada ya Katibu Mkuu huyo kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa makazi ya watumishi wa umma katika Kijiji cha Kijiweni, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi mkoani Lindi

Mwonekano wa jengo la mradi wa makazi ya watumishi wa umma lililopo katika Kijiji cha Kijiweni, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi mkoani Lindi.
Na Veronica Mwafisi-Lindi.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amekagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Umma unaojengwa katika Kijiji cha Kijiweni, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ili kuwasaidia watumishi hao kuwa karibu na ofisi wanazofanyia kazi kwa lengo la kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo leo, Katibu Mkuu Mkomi amesema ujenzi wa makazi ya watumishi hao utawasaidia kuepeukana na changamoto ya makazi ambayo imekuwa ikiwakabili na kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Amesema Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa ikiwajali sana watumishi wa umma katika kuboresha mazingira ya kazi ikiwemo utekelezaji wa mradi wa makazi ya watumishi.
“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kutekeleza kwa vitendo azma yake ya kuujenga utumishi wa umma pamoja na kuboresha mazingira ya utendaji kazi wa watumishi wa umma ili wawe na tija katika utoaji wa huduma kwa maendeleo ya taifa,” Katibu Mkuu Mkomi ameongeza.
Bw. Mkomi amesema mradi wa ujenzi wa makazi hayo ya watumishi upo katika hatua ya majaribio katika Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi ambapo pia unatekelezwa katika Mikoa ya Dodoma, Singida na Ruvuma.
Katibu Mkuu Mkomi katika ziara hiyo aliambatana na baadhi ya Wakurugenzi wa ofisi yake ambapo kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Bw. Patrick Allute amesema Watumishi Housing Investments ndiyo kandarasi inayojenga makazi katika mradi huo.
Bw. Allute ameongeza kuwa, mradi huo unafuatiliwa na kusimamiwa kikamilifu ili uweze kukamilika kwa wakati.





















.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
















