Tume ya Ushindani (FCC) imeweka mikakati mbalimbali ya kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi kwa wakati kwa kutumia mifumo ya kisasa katika utekelezaji wa majukumu yake, ikiwa ni sehemu ya kuongeza ufanisi na uwazi katika huduma za ushindani na biashara nchini.
Akizungumza wakati wa kikao kazi na watumishi wa Tume hiyo kilicholenga kupanga mikakati ya utekelezaji wa majukumu, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema hatua zinazochukuliwa na Tume zinalenga kuwahudumia wananchi kwa viwango vya juu vya ubora vinavyotambulika kitaifa na kimataifa.
Amesema FCC inaendelea kutekeleza dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuboresha mazingira ya biashara nchini kwa kuwashirikisha wafanyabiashara na wananchi kupitia mifumo rafiki, ya kisasa na yenye ufanisi katika utoaji wa huduma.
Bi. Ngasongwa amebainisha kuwa katika kipindi cha siku 100 za uongozi wa Rais Samia, FCC imechukua hatua za makusudi za kusogeza huduma karibu na wananchi, ikiwemo kuanzisha Ofisi ya FCC Mkoa wa Tanga pamoja na maeneo ya mipakani, hatua iliyolenga kuongeza wigo wa huduma na kuwafikia wananchi waliopo maeneo ya pembezoni.
Ameongeza kuwa FCC imeendelea kudumisha Cheti cha Ithibati ya Ubora ISO 9001:2015 kutokana na jitihada zake za kutoa huduma kwa weledi, uwazi na kuzingatia viwango vya ubora, huku akiwapongeza watumishi kwa juhudi zao katika kulinda hadhi ya taasisi hiyo.
Katika kikao hicho, watumishi walipata fursa ya kujadili na kutoa maoni kuhusu rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Tume wa miaka mitano (2026/27–2030/31), unaoakisi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050, sambamba na kuimarisha utamaduni wa ushirikishwaji katika maamuzi ya taasisi.
Kikao kazi hicho cha FCC kimefanyika Februari 2, 2026 katika ukumbi wa Hoteli ya Tiffany Diamond jijini Dar es Salaam.
Bw. Shalua Magandi, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi akichangia mada wakati wa kikao kazi na watumishi wa Tume, kilichofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Tiffany Diamond, Jijini Dar es Salaam Februari 02,2026.
Mwenyekiti wa Tughe Tawi la FCC, Bw. Emmanuel Ndyetabula akifuatilia kikao kazi cha Kaimu Mkurugenzi Mkuu na watumishi wa Tume, kilichofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Tiffany Diamond, Jijini Dar es Salaam Februari 02,2026.
Bi. Reticia Seni kutoka kampuni ya Dealer Ofisi ya Nganyila Lyapi Sweki, akihudumia wateja (hawapo pichani), waliokwenda kuuza dhahabu zao sokoni.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Katika hatua inayozidi kuipa nguvu ajenda ya ukuaji wa uchumi na maendeleo ya biashara nchini, Stanbic Bank Tanzania imeidhihirisha tena nafasi yake kama mdau muhimu wa masoko ya mitaji baada ya kushiriki kama Mratibu Mkuu wa Hatifungani ya Makazi iliyotolewa na First Housing Finance Tanzania (FHF), mpango unaofungua ukurasa mpya wa uwekezaji wa muda mrefu katika sekta ya makazi.
Hatifungani hiyo yenye thamani ya awali ya shilingi bilioni 5, ikiwa na chaguo la nyongeza ya shilingi bilioni 3, imepokelewa kwa mwitikio chanya kutoka kwa wawekezaji, ishara kuwa soko la mitaji nchini linaendelea kukua na kuaminiwa. Wachambuzi wa masuala ya fedha wanaeleza kuwa muundo wa hatifungani hiyo umebuniwa kwa umakini mkubwa, ukilenga kutoa faida za kifedha kwa wawekezaji huku ukiendeleza athari chanya kwa jamii.
First Housing Finance Tanzania, ambayo ni taasisi inayoongoza katika utoaji wa mikopo ya nyumba nje ya mfumo wa kawaida wa kibenki, imeendelea kuimarisha nafasi yake sokoni kwa kufikia asilimia 5.3 ya hisa ya soko la mikopo ya nyumba hadi Machi 31, 2025, na tayari imetoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 36 kwa mamia ya Watanzania.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Stanbic Bank Tanzania, Manzi Rwegasira, amesema hatifungani hiyo ni ushahidi kuwa masoko ya mitaji yanaweza kutumika kama chombo madhubuti cha kutatua changamoto halisi za kiuchumi.
“Makazi siyo tu paa juu ya kichwa; ni msingi wa familia imara, jamii zenye mshikamano na uchumi unaokua kwa kasi. Kupitia bidhaa za uwekezaji zilizo salama na zinazoaminika, tunaweza kuhamasisha mtaji na kuuelekeza kwenye maeneo yenye tija kubwa,” amesema Rwegasira.
Kwa mtazamo wa biashara, mapato yatakayopatikana kupitia hatifungani hiyo yataongeza uwezo wa FHF kutoa mikopo zaidi ya nyumba, hatua itakayoongeza wigo wa wateja, kukuza mapato ya taasisi hiyo na wakati huo huo kufungua minyororo mipya ya fursa katika sekta ya ujenzi, biashara ya vifaa vya ujenzi na huduma za kitaalamu.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kibenki kwa Makampuni na Uwekezaji wa Stanbic Bank Tanzania, Ester Manase, amesema uaminifu wa wawekezaji katika masoko ya mitaji hujengwa kupitia uwazi, uwajibikaji na nidhamu ya hali ya juu.
“Vyombo vya kifedha vinapaswa kuwa wazi, vinavyoeleweka na vinavyolingana na malengo ya muda mrefu ya uchumi. Hii ndiyo njia pekee ya kuyawezesha masoko ya mitaji kukua na kuvutia wawekezaji wengi zaidi,” amesema.
Naye Makamu Mkuu wa Rais wa Kitengo cha Masoko ya Mitaji na Usambazaji wa Madeni, Sarah Mkiramweni, amesema mpango huo unaendana kikamilifu na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050, ambayo inalenga kukuza uchumi jumuishi na ustawi wa jamii.
Kwa kuwalika wawekezaji wa ndani na nje kushiriki katika Hatifungani ya Makazi, Stanbic Bank Tanzania inaendelea kujiweka kama daraja muhimu kati ya mitaji na fursa, ikiimarisha nafasi yake katika kuleta mageuzi ya sekta ya fedha na kuchangia kwa vitendo maendeleo ya kiuchumi ya Tanzania.

Akihitimisha hotuba yake, Prof. Mkumbo aliwaalika wawekezaji wa Uingereza kuwa washirika wa karibu wa Tanzania katika kutekeleza Dira ya Taifa 2050, akisisitiza kwa msisitizo:
“Tuko wazi kwa biashara. Tunafanya mageuzi. Tunakua. Na tuko tayari kushirikiana.”
Kupitia mchango huo mpana, Stanbic inaendelea kuunga mkono ukuaji wa uchumi wa Tanzania kwa kuimarisha masoko ya mitaji na kuwezesha taasisi mbalimbali kupata njia bunifu na endelevu za ufadhili. Benki imeeleza kuwa itaendelea kuamini kuwa vyombo vya kifedha vilivyopangwa kwa umakini vina mchango mkubwa katika kuimarisha uthabiti wa kifedha na kukuza maendeleo ya muda mrefu ya taifa.














.jpeg)



























