Na Mwandishi Wetu.

Chuo Kikuu cha Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS) kimeendelea kuthibitisha ubora wake katika utafiti baada ya watafiti wake kadhaa kuingia katika orodha ya wanasayansi 20 bora nchini kwa mujibu wa AD Scientific Index ya mwaka 2026.

Kwa mujibu wa tangazo rasmi la chuo hicho, Profesa Mecky Matee ameongoza kwa kushika nafasi ya kwanza kitaifa, akifuatiwa na marehemu Profesa Ferdinand Mugusi aliyeshika nafasi ya saba. Wengine ni Profesa Sylvia Kaaya (nafasi ya 13), Profesa Karim Manji (nafasi ya 14), Profesa Bruno Sungunya (nafasi ya 15), pamoja na Profesa Eligius Lyamuya aliyeshika nafasi ya 17.

MUHAS imesema mafanikio hayo yanaakisi mchango mkubwa wa chuo hicho katika tafiti za afya, ubunifu wa kisayansi pamoja na juhudi zake za kuimarisha huduma za afya kitaifa na kimataifa.

Aidha, chuo hicho kimetoa heshima maalum kwa marehemu Profesa Ferdinand Mugusi, kikieleza kuwa mchango wake katika tafiti na malezi ya wataalamu utaendelea kuwa chachu ya maendeleo ya taaluma ya afya nchini.

Katika taarifa hiyo, MUHAS pia imewapongeza watafiti wengine wa chuo hicho waliotajwa katika viwango vya kitaifa, ikisisitiza kuwa juhudi zao zinaendelea kuimarisha hadhi ya taasisi hiyo katika jumuiya ya kitaaluma.

“Hongera sana kwa mafanikio haya makubwa, endeleeni kuinua kiwango,” ilisomeka sehemu ya ujumbe wa pongezi kutoka MUHAS.

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: