Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Washindi wa Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu kwa mwaka 2026 wametangazwa rasmi katika hafla iliyofanyika ukumbi wa The Superdome, Masaki jijini Dar es Salaam, huku waandishi mbalimbali wakitunukiwa kwa mchango wao katika kukuza na kuendeleza fasihi ya Kiswahili nchini.

Hafla hiyo iliyohudhuriwa na viongozi wa serikali, wasomi, pamoja na wadau wa sekta ya fasihi, ilishuhudia washindi wakikabidhiwa tuzo na mfano wa hundi za fedha kama ishara ya kuthamini ubunifu na juhudi zao katika uandishi.
Katika kipengele cha riwaya, Bishop John Hiluka aliibuka mshindi wa kwanza kupitia kazi yake “Waraka kutoka Gerezani”, akifuatiwa na Halfani Sudi aliyeshika nafasi ya pili kwa riwaya “Mnara wa Posta”. Nafasi ya tatu ilichukuliwa na Enock Maregesi kwa kazi yake “Alama za Bluu”.

Kwa upande wa ushairi, Abdalaj Salum Ngereza alitwaa ushindi wa kwanza kupitia diwani ya “Muwinda Elimu”, huku Kombo Abdalah Omar akishika nafasi ya pili kwa “Tunu ya Taifa”. Nafasi ya tatu ilikwenda kwa Hafidh Makame kwa diwani yake “Naisubiria Faraja”.
Katika kipengele cha hadithi za watoto, Amina Abdulrahman Mohamed aliibuka mshindi wa kwanza kwa kazi “Shumi na Vitungule”, wakati Fatma Suleiman akishika nafasi ya tatu kupitia hadithi “Kidau cha Panya”.

Kwa upande wa tamthilia, Hamis Kibari alitwaa nafasi ya kwanza kwa kazi yake “Ufalme wa Mabadiliko”, huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Esther Nyawale kwa tamthilia “Jiko la Ukombozi”.
Akizungumza katika hafla hiyo, mmoja wa waandaaji alieleza kuwa tuzo hizo zinaendelea kuwa chachu ya kuhamasisha ubunifu miongoni mwa waandishi wa Kiswahili, hususan kizazi kipya, na kuchangia kukuza lugha na utamaduni wa Mtanzania.

Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu ni miongoni mwa tuzo muhimu nchini zinazolenga kuenzi mchango wa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, katika kukuza lugha ya Kiswahili na fasihi yake.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: