Na Mwandishi Wetu

Balozi Sita zinazowakilisha nchi zao nchini Tanzania zimeshiriki Tamasha la Piano ya muziki wa Franco Rhumba kwa ajili kupata furaha.

Akizingumza wakati kufungua Tamasha hilo lilofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo nchini Tanzania Jean Pierre Massala amesema kuwa Muziki huo unakuwatanisha kupata furaha pamoja na kujenga umoja .

Amesema kuwa kuwa waandaji wameweza kuona umuhimu kukaa pamoja na kupata furaha kupitia muziki huo ambao unapendwa na Wakongo na Jamii zingine.

Massala amesema kuwa matamasha hayo hayo ni muhimu kwani yanakutanisha watu tofauti ambao wanafanya kujenga umoja wenye furaha.

Kwa upande wa Balozi wa Morocco nchini Tanzania Zakaria El Goumiri. amesema kuwa wameshiriki Tamasha hilo kufurahi na kutaka waandaji waendelee kuandaa kwani linawaweka pamoja

Aidha amesema kuwa furaha za muziki za muziki zinaunganisha makundi mbalimbali kwa kuleta upendo

Mmoja wa waandaji Tamasha hilo Alain Izai amesema kuwa wanashukuru mwitikio walioupata katika Tamasha kwa kuungwa na Balozi Sita Kushiriki mwanzo hadi mwisho.

Izai amesema kuwa wataendelea kuandaa matamasha hayo mara kwa mara katika kutoa burdani kujenga furaha katika nyoyo zao.

Hata hivyo amesema Muziki wa Rhumba unapendwa na kila rika ambapo kazi yao ni kuendelea kutunga katika kuboresha nyimbo za muziki huo.

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: