Waziri wa Madini Anthony Mavunde akizungumza leo wakati akifungua kikao kazi na Menejimenti ya Tume ya Madini Jijini Tanga.
Naibu Waziri wa Madini Dkt Steven Kiruswa akizungumza wakati wa kikao hiho

Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Mhandisi Yahaya Samamba akizungumza wakati wa kikao kazi hicho

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akizungumza

Na Oscar Assenga,TANGA

WAZIRI wa Madini Anthony Mavunde ameipongeza Tume ya Madini kwa kuvunja rekodi kukusanya kiasi cha Sh Bilioni 196 kwa kipindi cha siku 75 huku akieleza jambo hilo ni kubwa na inaonyesha wamedhamiria kuifanya sekta ya madini inachangia kwenye uchumi wa nchini.

Mavunde aliyasema hayo leo Jijini Tanga wakati akifungua kikao kazi na Menejimenti ya Tume ya Madini Jijini Tanga ambapo alisema kiwango hicho kimepokelewa mpaka leo 15 Septemba ndani ya miezi miwili ya mwaka huu na hilo linatokana na .

Alisema kiwango hicho kimeifanya kuvunja rekodi ya makusanyo ilihali mwaka 2015/2016 ilichukua mwaka mzima kukusanya Bilioni 161 lakini leo ndani ya siku 75 tume hiyo imeshakusanya kiasi hicho na hivyo kuvunja rekodi kwani waliojiwekea makusanyo ya Bilioni 60 mpaka Bilioni 65 kwa kila miezi na mwili iliyopita mmekusanya Bilioni 83 kila mwezi mmevuka malengo yao.

“Niwatie moyo na wakikaza buti na kuendelea na usimamizi huo mzuri na makusanyo wakifika mwakani mwezi wa saba watakuwa mmeandika historia kubwa”Alisema

Katika hatua nyengine Waziri Mavunde amewataka maafisa madini wakazi wa mikoa kuhakikisha wanashughulikia migogoro kwenye maeneo yao kwa haraka inapojitokeza badala ya kusubiri mpaka wafike viongozi wakubwa ikiwemo Waziri.

Alisema haiwezekani wao wapo kwenye mikoa na wanashindwa kutatua migogoro iliyopo hivyo wabadilike wahakikishe wanaishughulia na utatuzi wake unapatikana haraka bila kumuonea mtu.

Alisema anajisikia vibaya kuona mgogoro inapotokea mpaka aende waziri au Naibu Waziri wakati wapo maafisa madini wakazi mpaka umshinde ndio uvuke uende ngazi lakini kazi yenu hya kwanza ni utatuzi wa migogoro labda mniembie nyie ni sehemu ya migogoro lakini kama sio sehemu ya migogoro tatueni migogoro,

“Niwaambieni kipimo chenu cha kazi kitakuwa ni namna mnavyotatua migogoro tatueni na sio mpaka msubiri ufike hatua ya juu anzeni nao lakini mtatue migogoro katika haki asionewe mtu simamieni haki ndugu zangu”Alisema Waziri Mavunde

Udhibiti wa Utoroshwaji wa Madini

WAZIRI Mavunde aliwataka maafisa hao kuhakikisha wanadhibiti utoroshwaji wa madini katika maeneo yao hususani ile ya mipakani

“Mmeona hivi karibuni kuna kesi nyingi sana zinapelekwa mahakamani na juzi tumewakamata watu Bandari Dar na kilo 15 za dhahabu na tumezitaifisha ela dhahabu na wanakwenda mahakamani,huko kwenye maeneo yenu hakikisheni mnashirikiana kwenye task force kudhibiti hili lisitokee”Alisema Waziri Mavunde

Aidha Waziri Mavunde aliutaja Mkoa wa Madini wa Kahama ndio unaongoza kwa shughuli za za utoroshaji wa madini na mbinu hivi sasa zimebadilika wanasikie wale ambao wanakwenda kuuziana kwenye mashine za Mpunga ambapo alimtaka Afisa Madini Mkazi wa Mkoa huo kuhakikisha anaimarisha eneo hilo.



Katika hatua nyengine Waziri Mavunde amewataka maafisa madini wakazi wa mikoa kuhakikisha wanashughulikia migogoro kwenye maeneo yao kwa haraka inapojitokeza badala ya kusubiri mpaka wafike viongozi wakubwa ikiwemo Waziri.

Mavunde alitoa agizo hilo leo Jijini Tanga ambapo alisema haiwezekani wao wapo kwenye mikoa na wanashindwa kutatua migogoro iliyopo hivyo wabadilike wahakikishe wanaishughulia na utatuzi wake unapatikana haraka bila kumuonea mtu.

Alisema anajisikia vibaya kuona mgogoro inapotokea mpaka aende waziri au Naibu Waziri wakati wapo maafisa madini wakazi mpaka umshinde ndio uvuke uende ngazi lakini kazi yenu hya kwanza ni utatuzi wa migogoro labda mniembie nyie ni sehemu ya migogoro lakini kama sio sehemu ya migogoro tatueni migogoro,

“Niwaambieni kipimo chenu cha kazi kitakuwa ni namna mnavyotatua migogoro tatueni na sio mpaka msubiri ufike hatua ya juu anzeni nao lakini mtatue migogoro katika haki asionewe mtu simamieni haki ndugu zangu”Alisema Waziri Mavunde

Udhibiti wa Utoroshwaji wa Madini

WAZIRI Mavunde aliwataka maafisa hao kuhakikisha wanadhibiti utoroshwaji wa madini katika maeneo yao hususani ile ya mipakani

“Mmeona hivi karibuni kuna kesi nyingi sana zinapelekwa mahakamani na juzi tumewakamata watu Bandari Dar na kilo 15 za dhahabu na tumezitaifisha ela dhahabu na wanakwenda mahakamani,huko kwenye maeneo yenu hakikisheni mnashirikiana kwenye task force kudhibiti hili lisitokee”Alisema Waziri Mavunde

Aidha Waziri Mavunde aliutaja Mkoa wa Madini wa Kahama ndio unaongoza kwa shughuli za za utoroshaji wa madini na mbinu hivi sasa zimebadilika wanasikie wale ambao wanakwenda kuuziana kwenye mashine za Mpunga ambapo alimtaka Afisa Madini Mkazi wa Mkoa huo kuhakikisha anaimarisha eneo hilo.

“Lakini pia nimemwambia Katibu Mkuu waifanye Kahama kama Kanda Maalumu kwa maana dhahabu nyingi inatoroshewa kupitia Kahama nimekuona RMO mara mbili mara tatu mnatoka mnakamata endeleee na mikoa mingine hasa mikoa ya Mipakani”Alisema Waziri huyo.

Waziri huyo aliwataka maafisa hao kila mmoja katika eneo lake ahakikishe anakuwa sehemu ya udhibti wa utoroshaji wa madini kwa maana utoroshwaji huo unasababisha kupoteza mapato mengi.

Hata hivyo Waziri huyo aliitaka Ofisi ya Kamishna wa Madini kushirikiana na RMO kuwalea wachimbaji wadogo na kuwaendeleza katibu mkuu pale wizara wawekezaji wakubwa wana meneja wake ndani ya wizara wa kuyasimamia katibu mkuu kupitia Ofisi ya Kamishna natoa maelekezo tengenezeni utaratibu kushirikiana na RMO kuwaibua watanzania wawekezaji wa sekta ya madini kupitia ofisi ya Kamishna wawelee nao wagraduate kutokana na kwamba hivi sasa wenyewe hawana muangalizi.

Alisema ili siku moja waweze kutengeneza mabilioni wengi kupitia wachimbaji wadogo hivyo wakikaa nao na kuwasaidia kama wanavikwazo waone namna ya kuyatatua ili kuweza kuongeza mapato.

Katika hatua nyengine Waziri Mavunde aliwataka kuhakikisha wanadhibiti upotevu wa mapato waende wakazibe mianya na makusanyo yaweze kuongezeke huku akieleza hiyo ni sehemu ya kazi yako ya msingi.

“RMOs kila mtu amewekewa malengo ya kuwafikia kwa mwaka wa fedha huu kama unahisi kwako unashindwa kufikia malengo kwa jambo ambalo halihusiani na wewe ni tatizo la kimfumo, kimundo lipo nje ya uwezo.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: