Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akizungumza wakati akikagua nyumba 10 za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la Kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga leo Jumanne Julai 10,2019.Kulia ni Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Richard Abwao,kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Muonekano wa nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la Kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Muonekano wa nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.


Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akikagua nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akikagua nyumba za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro akisamiliana na waendesha bodaboda katika eneo la nyumba za makazi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga na kuwakumbusha kuzingatia sheria za usalama barabarani na kuwasihi kuacha kubeba mishikaki,wavae kofia ngumu na wawe na leseni. 

Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini Tanzania Simon Sirro ametembelea na kukagua nyumba 10 za kisasa za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la Kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga na kugharimu shilingi milioni 225.

Mkuu huyo wa jeshi la polisi amekagua nyumba hizo leo Jumanne,Julai 10,2019 na kueleza kuridhishwa jinsi zilivyojengwa kwa umaridadi na ubora wa hali ya juu. 

Nyumba hizo 10 ni sehemu ya nyumba 114 ambazo ujenzi wake umekamilika nchi nzima ikiwa ni sehemu ya nyumba 400 zinazojengwa maeneo mbalimbali nchini kwa ajili ya makazi ya askari polisi.

"Ujenzi huu umegharimu shilingi milioni 225,ni kweli nyumba hizi ni nzuri sana,nimpongeze sana Mhe. Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe.Zainab Telack na kamati yake ya ulinzi na usalama,kamati ya ujenzi na wadau wote walioshiriki kwa kazi hii nzuri"

"Sasa tunamsubiri Mhe. Rais,Dkt.John Pombe Magufuli muda siyo mrefu atazindua hizi nyumba 114 nchi nzima. Pesa zilizotolewa ni kwa ajili ya kujenga nyumba 400,lakini mpaka sasa zilizokamilika sasa ni 114",alisema IGP Sirro. 

Kwa upande wake,Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack alimshukuru Rais Magufuli kwa kutoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa makazi ya askari polisi huku akimuomba IGP Sirro kutafuta pesa kwa ajili ya ukarabati wa baadhi ya nyumba za askari ambazo hali yake siyo nzuri.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: