Ameandika Askofu Benson Bagonza (PhD)

Kuna maswali magumu mbele yetu baada ya bunge kupitisha uamuzi wa kihistoria tarehe 2 Aprili 2019.

1. Je, Bunge limepitisha azimio la kutofanya kazi na Prof. Assad au na CAG?

2. Kama ni Prof Assad, basi Bunge bado linaweza kufanya kazi na CAG Assad.

3. Kama Bunge halitafanya kazi na CAG, linamuingiza Rais ktk mgogoro mkubwa wa Kikatiba, kwa sababu:

- Ndani ya siku 7 tangu kupokea Ripoti ya CAG, Rais anatakiwa kuipeleka Ripoti Bungeni iliyofanywa Kazi na CAG ambaye ni Prof. Assad.

4. Asipoileta atakuwa amevunja Katiba ya Nchi aliyoapa kuilinda.

5. Akiileta, atakuwa amelidharau Bunge wakati naye ni sehemu ya Bunge.

6. Akiteua CAG mwingine, huyo mpya hatakagua upya bali ataleta iliyokaguliwa na CAG Prof. Assad ambaye hatakiwi Bungeni.

7. Katiba inatamka kuwa; mchakato wa kumuondoa CAG ni mrefu na iko kimya kuhusu kuendesha mchakato wakati kuna Kaimu CAG.

Ukiwahi kuzaliwa unaona mengi. Ukiwahi kufa unakosa mengi.

Dumisha Uhuru na Umoja.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: