Ujumbe huu ameuandika katika ukurasa wake wa Instagram

Na Steve Nyerere2

Kwanza nichukue fursa hii kuipongeza Azam Cinema Zetu kwa ubunifu mzuri kwenye suala hili la kuwatunuku wasanii wa filamu wanaofanya vizuri kwenye tasnia hii ya filamu Nchini.

Lakini pili, nitoe pongezi kwa wasanii wote ambao walishiriki kwenye ushindani wa Tuzo hizi za Cinema Zetu hapo jana (Jumamosi Februari 23, 2019).

Katika jambo lolote lile suala la utaratibu ni jambo muhimu sana kufatwa na hakuna anayebisha kwenye hili, ila huo utaratibu lazima uwende na uhalisia.

Jana yametokea mengi sana ya kufurahisha na kusikitisha kwenye Tuzo zetu ambazo zimeanza kuchukua umaarufu mkubwa hapa nchini.

Tunajua jambo hili bado ni geni kwenu Azam na tunaamini kabisa bado mna nafasi ya kulifanya kuwa bora kabisa na lenye heshima kubwa sana kwa Azam, Wasanii na Taifa kwa ujumla.

Mimi leo nataka nizungumzie maeneo matatu tu na ikiwapendeza mnaweza kurekebisha.

Kwanza, namna ya utoaji tuzo zenyewe, nani anashindanishwa na nani. Huwezi kusema msanii bora wa kike au wa kiume ukawashindanisha wasanii wakongwe na wasanii ambao wamecheza movie moja tu na hapohapo huyo aliyecheza movie moja ameshinda.

HAPANA lazima kuna sehemu mlikosea waandaji, na mnaweza kumpa mtu bichwa akajiona yeye ni msanii mkubwa sana maana ameshindanishwa na msanii mkubwa sana na amemshinda wakati kiuhalisia hawafanani hata kidogo kiuwezo na kila kitu.

Mimi nahisi mngeongeza vipengele hata cha msanii bora anayechipukia na siyo kufanya kama mlichokifanya jana kwangu mm naona kama ni udhalilishaji.

Hapa lazima waandaji mkae na kujitathmini maana watu wakichukizwa na jambo linalofanywa na kituo kikubwa kama Azam linaweza kusababishia watu kuichukia na brand yenyewe ya Azam kwahiyo umakini kwenye hili jambo unatakiwa uwe mkubwa sana. Lakini pia kwenye hili si vibaya nyie mkawa wasimamizi wakuu lakini mkachukua watu maalum wa kuwasimamia kitaalam zaidi maana mkitaka mfanye kila kitu nyie mnafeli, msichukulie kila kitu ni rahisi (simple) au kubana matumizi NO, chukueni wataalamu wa kuandaa shughuli kubwa kama hizi au kwa kizungu wanasema ku (outsource ) wabobezi wa shughuli kubwa kama hizi na wanakuwa na nyinyi kuanzia mwanzo wa maandalizi mpak mwisho hili naomba mlifanyie kazi.

Pili, haiwezekani watu wakajaa vile mpaka wakakosa viti WHY? Kama kadi
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: