KATIBU Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua,(watatu kulia), akizungumza na vyombo vya habari mbele ya mashine (turbine) ya kufua umeme inayofanyiwa matengenezo makubwa ya kujilinda kwenye kituo cha kufua umeme wa gesi asilia cha Ubungo II, jijini Dar es Salaam.
Dkt.Mwinyimvua (wapili kushoto), na Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga, (kulia), wakiongozwa na Meneja Miradi wa TANESCO, Mhandisi Stephene Manda, (kushoto), walipotembelea kuona transfoma hiyo.
Hii ndiyo transfoma kubwa mpya yenye uwezo wa kusukuma umeme wa Megawati 240, ambayo inafungwa kwenye Kituo kikuu cha kupoza na kusambaza umeme cha Ubungo na hivyo kufanya kituo hicho kuwa na transfoma tata.
Wataalamu wakiwa kwenye chumba cha SCADA wakifuatilia mwenendo wa umeme kutoka vyanzo na vituo mbalimbali vya umeme nchini. Kituo hiki kiko Ungungo.
Meneja wa Kituo cha kufua umeme utokanao na gesi asilia cha Ubungo II, Mhandisi Lucas Busunge, (kushoto), akifafanua jambo mbele ya Katibu Mkuu, Dkt. Mwinyimvua (wapili kulia) na Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga, (watatu kushoto).
Mhandisi wa TANESCO ambaye anahudumu kwenye chumba cha udhibiti (control room) cha kituo kikuu cha kupoza na kusambaza umeme cha Ubungo akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu na ujumbe wake, walipotembelea kituo hicho leo Februari 26, 2019.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: