Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola (Mb), akizungumza na Makamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kabla ya kufungua rasmi Kikao cha Makamanda wa Jeshi hilo katika ukumbi wa Bwaro la FFU, Jijini Dodoma.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, CGF Thobias Andengenye, akisoma hotuba ya kumkaribisha Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola (Mb), katika Kikao cha Makamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, katika ukumbi wa Bwaro la FFu, Jijini Dodoma.
 Baadhi ya Makamanda wa Mikoa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakimsikiliza, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola (Mb), wakati akizungumza kabla ya kufungua rasmi Kikao cha Makamanda wa Jeshi hilo katika ukumbi wa Bwaro la FFU, Jijini Dodoma.
 Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Billy Mwakatage akimshukuru Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola (Mb), mara baada ya kufungua rasmi Kikao cha Makamanda wa Jeshi hilo katika ukumbi wa Bwaro la FFU, Jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola (Mb), akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya wa Dodoma Patrobas Katambi (watatu kulia), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima (wapili kulia), Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (wapili kushoto), Makamishna na Makamanda wa Mikoa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, mara baada kufungua rasmi Kikao cha Makamanda wa Jeshi hilo katika ukumbi wa Bwaro la FFU, Jijini Dodoma (Picha zote na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji).
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: