Msanii wa muziki wa kizazi kipya Amini Mwinyimkuu amesema kuwa hayupo tayari kumuoa mwanadada Linah Sanga hata kama mlisema amemuimbia wimbo.

Akizungumza jijini Dar na mdaku wetu msanii huyo alisema kuwa watu wengi wamesema juu ya kumuoa Linnah kutonana na gumzo la wimbo wake mpya wa 'Novemba/Disemba' kuwa ni fumbo la harusi yake ambayo amepanga ifanyike kipindi hicho.

Mdaku wetu alidadavua kuwa Amini aliweka wazi kuwa kila kitu kinaenda kwa mipango ila kwa sasa hayupo tayari kuweka wazi kila kitu maana mengine hubaki kifamilia.

'Mniache jamani nipumue wimbo wangu wa 'Novemba/Disemba' msubirie utoe majibu tu, mnayoyataka nyie wenyewe wala msinyumbishwe na maneno ya watu, alisema Amini.

Mnamo mwezi Januari msanii Amini alitoa wimbo wa 'Novemba/Desimba' na kuwa gumzo mpaka mitaani wengine wakasema amemuimbia Linnah, mara oh! Anataka kuona miezi hiyo aliyoitaja...basi ikawa vurugu mechi midomoni mwa watu.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: