Pichani ni Kamati ya maandalizi ya shindano la utunzi kutoka taasisi ya Tanzania Gatsby Trust (TGT), kutoka ni Mwenyekiti Ibrahim Seushi (kulia) na Mjumbe wa kamati, Profesa Mugyabuso Mlinzi Mulokozi ambaye alikuwa akionyesha picha ya mwasisi wa utunzi.

Kamati ya usimamizi wa Tunzo ya ushairi ya Ibrahim Hussein, kwa kushirikiana na Tanzania Gatsby Trust (TGT) na Mkuki na Nyota, imezindua shindano jipya la ushahiri.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo katika ukumbi wa Idara Maelezo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti Ibrahim Seushi alisema kuwa lengo kuu la shindano hilo linafanyika ili kumuenzi mwakilishi wa Tunzo, Marehemu Gerald Belkin ambaye alikuwa mpiga filamu wa Canada aliyeoshi nchini Tanzania katika miaka 1970. Bwana Belkin aliipenda lugha na fasihi ya Kiswahili na alifanya kazi na mtunzi Ebrahim Hussein kuikuza. Alichangia mfuko akitaka uwe chachu ya kuendeleza Kiswahili, hasa utunzi wa mashairi.

Tanzania Gatsby Trust (TGT) ambalo ni shirika linalosimamia mfumo huu, imewashirikisha wajumbe wa kamati kutoka wachapishaji Mkuki na Nyota pamoja na wananzuoni mbalimbali wa ushairi katika kuendesha shindano hili lililofunguliwa leo Februari 26.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: