Familia ya Linah ni ya kidini kutokana na ukweli kuwa baba mzazi wa Linah ni mchungaji wa kanisa .
Familia yake ina jumla ya watoto watano wakati Linah akiwa mtoto wa tatu kuzaliwa kutoka kwenye familia ya Mzee Sanga.
Familia anayotokea Linah ni familia iliyojaa wanafamilia waliojaa vipaji wenye vipaji vya kuimba.

MAISHA BINAFSI;

Linah ana anarafiki wa kiume ‘boyfriend’ ambaye ni mwana muziki mwenzake Amini, anaishi peke yake maeneo ya Kinondoni ambapo amepanga chumba.

Mbali na muziki pia Linah pia ni muigizaji kwani kwa sasa amesaini mkataba wa na clouds Tv ambako ataonekana katika tamthilia inayokwenda kwa jina la ‘69 Records’ ambayo itakuwa inarushwa na Clouds Tv.

MIPANGO YA BAADAE YA LINAH KIMUZIKI.

Mpango mkubwa na wa kwanza wa linah ni kurudi shule,na hii ni kutokana na ukweli kuwa yeye aliishia kidato cha nne tu,jambo lililochangiwa kwa kiasi kikubwa na matatizo yake ya kiafya.

Kama hiyo haitoshi pia Linah amepanga kukuza muziki wake na malengo yake ni kuufanya ujulikane Afrika nzima na Duniani kote.

MAISHA KABLA YA UIMBAJI

Kabla yakuanza uimbaji Lina alikuwa anajishughulisha na uimbaji wa nyimbo za injili lakini sehemu kubwa ya maisha yake ilikuwa ni shule kwa sababu ameanza muziki rasmi muda mfupi baada ya kumaliza shule.

Sikiliza nyimbo yake ya Lonely inayotamba kwa sasa...

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: