Je, una watu? Kama huna, jitahidi kutengeneza watu.
1. Siku ukikumbwa na kesi au kupelekwa mahabusu, una watu wa kukusaidia au ni mwisho wa safari? Kama huna, tengeneza watu.
2. Siku ukilazwa hospitali, una watu wa kukuletea msaada wa chakula na bili? Kama huna, tengeneza watu.
3. Siku unapokwama hata nauli ya chakula, una mtu wa kukukopesha hata kidogo? Kama huna, tafuta watu.
4. Siku unapofukuzwa kwenye nyumba, una watu wa kunusuru mali zako? Kama huna, tengeneza watu.
5. Siku unapokamatwa kwa kosa barabarani, una mtu wa kukushauri au kukusaidia kisheria? Kama huna, tengeneza watu.
6. Nafasi za ajira zinapotangazwa (polisi, jeshi, ualimu n.k.), una watu wa kukupa taarifa sahihi na kukushauri? Kama huna, tengeneza watu.
7. Unapodhulumiwa mali zako, una watu wa kukulinda na kukusimamia? Kama huna, tafuta watu.
8. Una sifa zote za kupandishwa cheo au kuteuliwa, lakini una watu wa kukusemea? Kama huna, tengeneza watu.
9. Unapobambikiziwa kesi nzito, una watu wa kukusaidia kutafuta haki? Kama huna, tengeneza watu.
10. Unapoanzisha au kupanua biashara, una watu wa kukufungulia milango na kupunguza vikwazo? Kama huna, tafuta watu.
Ukweli ni kwamba dunia hii inaendeshwa kwa watu.
Elimu bila mtandao wa watu mara nyingi haina matokeo makubwa. Biashara bila watu haisongi. Siasa bila watu hukwama. Kipaji bila watu hufifia. Mafanikio bila watu ni ndoto ngumu kufikia.
Watu ni maisha. Watu ni mtaji. Watu ni fursa.
Hakikisha una watu serikalini, mtaani, hospitalini, mahakamani, kazini, kwenye biashara, na hata nje ya nchi.
Huo ndio mtandao wa mahusiano — kwa Kiingereza huitwa connection.
Jenga mahusiano, linda watu wako, heshimu watu — utapunguza kwa kiasi kikubwa ugumu wa maisha.



Toa Maoni Yako:
0 comments: