Na Mwandishi Wetu – Dodoma.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeendelea na mchakato wake wa ndani wa kuwachuja wagombea wa nafasi za ubunge kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025, ambapo orodha ya awali imebainisha jumla ya wabunge 27 wa sasa kutoka majimbo mbalimbali ya Tanzania Bara ambao hawakuteuliwa kuendelea katika hatua ya kupigiwa kura za maoni.

Wabunge hao ni miongoni mwa wale waliokuwa wakihudumu katika majimbo yao kuanzia mwaka 2020 lakini sasa hawakupitishwa katika hatua ya awali ya mchujo, hali inayoashiria mabadiliko makubwa ndani ya chama kuelekea uchaguzi ujao.

Orodha kamili ya Wabunge waliokosa uteuzi wa awali ni kama ifuatavyo:

  1. Mhe. Mrisho Mashaka Gambo – Arusha Mjini

  2. Mhe. Emanuel Ole Shangai – Ngorongoro

  3. Mhe. Mohamed Lujuo Moni – Chemba

  4. Mhe. Nicodemus Maganga – Mbogwe

  5. Mhe. Justine Nyamoga – Kilolo

  6. Mhe. Stephen Byabato – Bukoba Mjini

  7. Mhe. George Ndaisaba Ruhoro – Ngara

  8. Mhe. Zuberi Mohammed Kuchauka – Liwale

  9. Mhe. Pauline Gekul – Babati Mjini

  10. Mhe. Flatey Maasai – Mbulu Vijijini

  11. Mhe. Christopher Ole Sendeka – Simanjiro

  12. Mhe. Vedastus Matayo Manyinyi – Musoma Mjini

  13. Mhe. Luhaga Joelson Mpina – Kisesa

  14. Mhe. Godwin Kunambi – Mlimba

  15. Mhe. Geoffrey Mwambe – Masasi

  16. Mhe. Cecil Mwambe – Ndanda

  17. Mhe. Anjelina Mabula – Ilemela

  18. Mhe. Mansour Shanif Hirani – Kwimba

  19. Mhe. Hassan Zidadu Kungu – Tunduru Kaskazini

  20. Mhe. Iddi Mpakate – Tunduru Kusini

  21. Mhe. Iddi Kassim Iddi – Msalala

  22. Mhe. George Mwenisongole – Mbozi

  23. Mhe. Seif Hamisi Gulamali – Manonga

  24. Mhe. Omar Shekilindi – Lushoto

  25. Mhe. Januari Makamba – Bumbuli

  26. Mhe. Alfred Kimea – Korogwe Mjini

  27. Mhe. Twaha Mpembenwe – Kibiti

Kwa mujibu wa vyanzo vya ndani ya chama, mchakato wa uteuzi unalenga kuwapa nafasi wagombea wenye mvuto zaidi kwa wapiga kura, weledi na wale watakaoweza kutekeleza ilani ya chama kwa ufanisi mkubwa.

Hali hii inaonyesha dhamira ya CCM ya kufanya mabadiliko na kusikiliza sauti ya wananchi katika ngazi za chini kwa kuhakikisha wagombea wake wanakidhi matarajio ya wapiga kura.

Mchakato wa kura za maoni unatarajiwa kuendelea kwa mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani huku macho yote yakiwa kwa wagombea watakaoibuka kidedea kupeperusha bendera ya chama hicho tawala katika Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Je, watarudi kwa tiketi nyingine? Je, majimbo yao yatazidi kubaki CCM? Tafakari.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: