Lipo la kujifunza katika utumishi wetu, Picha inajieleza, Kobra na Chatu kila Mmoja ni chanzo cha kifo Kwa mwenzake ingawa wote ni nyoka. Chatu kamuua Kobra Kwa kumyonga na Kobra kamuua Chatu Kwa kumng'ata. Mmoja kakosa hewa mwingine kadungwa Sumu na wote wamekufa. 

 Hivi ndivyo watu tunamalizana, urafiki unakwisha, mahusiano yanavunjika, familia zinasambaratika, taasisi zinakufa na kila upande kuumia kwa sababu ya kila Mmoja kutaka kuwa bora zaidi ya mwingine, wengine, kutaka kuoneshana umwamba au utemi! Wengine kuumizana kwa uzushi, umbea, kuwekeana maneno na kutengenezeana ajali, kuvuana nguo, kudhalilishana, kudhulumiana, ama kukwamishana kimajukumu mpaka wanaharibiana wote. 

Tafakari kabla ya kubeba dhamana ya kumfanyia mwenzako jambo la ovyo, tafakari dhamana yako na ya mwenzako kabla hamjafanyiana mambo yasiyo na tija. Tukumbuke, Sote tuna dhamana kila Mmoja kwa nafasi yake. 

Mwenyezi Mungu atusaidie kuyafahamu haya na kuyatenda kwa wema!
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: