Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, alipokuwa akiuwaga Mwili wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu,katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani,Mnazi mmoja Mjini Unguja leo asubuhi, Marehemu alifariki juzi Jijini Dae es Salaam, na atazikwa Kijiji kwao Mbuzini Wilaya Magharibi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimpa pole Mjane wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu,Mama Miriam Sepetu, alipofika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani, Mnazi mmoja Mjini Unguja, kuuaga mwili wa Marehemu leo Asubuhi.
Baadhi ya Wananchi mbali mbali wakiwa katika sehemu maalum nje ya ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani, Mnazi mmoja Mjini Unguja,wakisubiri kuuaga mwili wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu, leo asubuhi ambapo utazikwa Kijiji kwao Mbuzini Wilaya Magharibi.

Picha na Ramadhan Othman, Ikulu.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

1 comments:

  1. Mungu alitoa na atimaye ametwa.Jina lake libarikiwe.

    ReplyDelete