
Lakini ukweli ni kwamba tumeelekeza macho yetu kwa Haiti kama Taifa, tumesahau shida zinazowakumba Wa-Haiti kama mtu mmojammoja. Katika picha hii unaweza kuona mama huyu akinyang'anywa bidhaa zake za msaada alizopatiwa na wasamaria wema. Wanaomnyang'anya huwezi kuwaita wezi, ni waathirika wenzake. Ukweli ni kwamba hali ya usalama katika Haiti, ukiacha janga la tetemeko, ni mtihani mkubwa kwa serikali ya Haiti, na wananchi hawako salama sana. Hali inapofikia namna hii hatuna budi, japo kwa sekunde 10 kila siku, kusema "Muumba elekeza macho yako kwa watu wa Haiti, Amen."
Picha na AFP
Toa Maoni Yako:
0 comments: