Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Kampuni ya Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo ya jamii na uchumi wa ndani kupitia kampeni yake ya Cheers to Bars, inayotambua mchango mkubwa wa baa katika kuwaleta watu pamoja, kukuza biashara ndogo ndogo na kuimarisha shughuli za kiuchumi nchini.

TBL imesema kuwa baa zimekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku ya Watanzania, zikitoa nafasi kwa marafiki na majirani kukutana, mashabiki wa soka kushuhudia mechi pamoja na wafanyabiashara wadogo kuendesha shughuli zao. Kampeni hiyo inalenga kuzisherehekea baa kwa mchango wake katika kujenga mshikamano wa kijamii na kuchochea maendeleo ya uchumi.

Mbali na kuwa sehemu za burudani, TBL imeeleza kuwa baa zimeendelea kutoa ajira kwa maelfu ya Watanzania, wakiwemo wamiliki wa baa, wahudumu, wauzaji wa chakula, wasambazaji wa bidhaa, walinzi, wasafishaji pamoja na watoa huduma za usafiri, hali inayochangia kuongeza kipato kwa watu wengi na kuimarisha mzunguko wa fedha katika jamii.

Kampeni ya Cheers to Bars pia imeangazia nafasi ya baa wakati wa matukio makubwa ya michezo, hususan soka, ambapo mashabiki wengi hupendelea kutazama mechi kwa pamoja katika mazingira yanayowapa fursa ya kushirikiana, kushangilia na kujenga kumbukumbu za pamoja.

Hali hiyo ilijidhihirisha katika Baa ya Kitambaa Cheupe jijini Dar es Salaam, ambapo mashabiki walikusanyika kushuhudia mechi ya robo fainali kati ya Hispania na Ubelgiji. Mechi hiyo iligeuka kuwa zaidi ya mchezo wa soka, huku ikiunganisha watu wa kada mbalimbali walioshiriki kushangilia na kufurahia burudani kwa pamoja.
Akizungumza kuhusu kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Sheria na Masuala ya Ushirika wa TBL, Neema Temba, alisema Cheers to Bars si kampeni inayolenga soka pekee, bali ni jukwaa la kutambua mchango wa baa na watu wanaoziendesha katika maendeleo ya jamii na uchumi wa Tanzania.

"Baa ni sehemu muhimu ya maisha ya kijamii na kiuchumi ya Watanzania. Zinasaidia kujenga maisha ya watu, zinatoa fursa kwa biashara ndogo ndogo na zinatoa nafasi kwa jamii kukutana na kuimarisha mahusiano. Kupitia Cheers to Bars, tunazisherehekea baa hizi pamoja na watu wanaoziendesha, huku tukiwahamasisha watumiaji kufurahia vinywaji kwa kuwajibika," alisema Neema.
Aliongeza kuwa wakati wa mechi kubwa za soka, shughuli za biashara huongezeka kwa kiasi kikubwa katika baa na maeneo yanayozizunguka. Wauzaji wa chakula, wasambazaji wa bidhaa, madereva wa usafiri na watoa huduma wengine wote hunufaika kutokana na ongezeko la wateja, jambo linaloifanya sekta ya ukarimu kuwa kichocheo muhimu cha uchumi wa ndani.

Kwa mujibu wa TBL, mafanikio ya kampeni hiyo yanaonesha kuwa baa za kienyeji zimeendelea kuwa sehemu muhimu zinazochangia maendeleo ya jamii kwa kuunganisha watu kupitia michezo na burudani, huku zikitoa fursa za ajira na biashara kwa makundi mbalimbali.

Kampuni hiyo imewataka Watanzania kuendelea kuunga mkono baa za kienyeji na kushiriki burudani katika mazingira salama kwa kutumia vinywaji kwa uwajibikaji. TBL imeeleza kuwa itaendelea kutekeleza kampeni ya Cheers to Bars kama sehemu ya juhudi zake za kuthamini mchango wa baa katika ukuaji wa uchumi, maendeleo ya jamii na ustawi wa sekta ya ukarimu nchini.

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: