Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Tasnia ya burudani nchini imegubikwa na majonzi makubwa baada ya msanii na mshereheshaji mashuhuri, Emmanuel Mathias ‘MC Pilipili’, kufariki dunia ghafla leo mchana wakati akiwa safarini kuelekea jijini Dodoma kwa ajili ya shughuli za kazi.

Taarifa za kifo chake zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii majira ya saa moja jioni kupitia ujumbe kutoka kwa baadhi ya watu wake wa karibu, zikizua wasiwasi na maswali mengi kutoka kwa mashabiki na wadau wa sanaa.

Akithibitisha msiba huo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya General jijini Dodoma, Dkt. Ernest Ibenzi, amesema MC Pilipili alifikishwa hospitalini hapo tayari akiwa ameshafariki dunia.

“Ni kweli tumempokea akiwa tayari amefariki,” alisema kwa kifupi Dkt. Ibenzi, akibainisha kuwa taratibu za kitabibu zinaendelea.

MC Pilipili alikuwa mmoja wa vipaji vilivyochangamsha sanaa ya uchekeshaji na ushereheshaji nchini, na kifo chake kimeacha pengo kubwa kwa mashabiki na wenzake katika tasnia.

Familia yake inatarajia kutoa taarifa zaidi kuhusu mipango ya mazishi na hatua nyingine za maombolezo.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: