Nianze kwa kutoa pongezi za dhati kwa Mtandao wa Vodacom Tanzania kwa kuweza kufanikisha zoezi la usajili wa alama za vidole likawa jepesi kwa kuwafuata wateja katika mitaa mbali mbali hapa jijini Dar es Salaam.

Hili jambo nimelishuhudia mwenyewe jinsi vijana wanavyoingia mtaani na kusajili wananchi bila ya kuwatoza pesa yeyote.

Jambo lililonishangaza ni baadhi ya mitandao ya simu za mkononi kuwatoza pesa wananchi pindi wanapotaka kukamilisha usajili wao kwa alama za vidole.

Hili sikubalini nalo nalipinga na ndiyo maana nimeandika waraka huu wa wazi kwa viongozi ili watambue vijana wao wanayoyafanya mtaani.

Inawezekanaje ukamtoza mwananchi Tsh 1,000 kwa mtandao mmoja wa simu alionao??? wakati hili zoezi lilitangazwa na serikali ni bure??? Jambo hili nimelishuhudia baada ya kuwaomba vijana wanisajili walipomaliza nikaambiwa nitoe Tsh 2,000 kwa vile walinisajilia laini zangu mbili nilikataa na wakaanza lalamika nikawambia hili zoezi halipaswi kutozwa mwananchi yeyote, waondoka shingo upande.

Basi niwaombe wahusika wa mitandao ya simu ya Airtel, Tigo na TTCL kuonya vijana waache kutoza pesa ili kuwakamilishia wananchi zoezi la alama za vidole.

Tunaiomba mamlaka husika hasa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kukemea mara moja mchezo unaofanywa na vijana ambao ameona ndiyo njia pekee ya kujipatia pesa.

Ni Mimi Blasio Kachuchu.
Mkazi wa Mbezi Makabe-Dar es Salaam.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: