Na Amini Mgheni.

Ndio, wakati umefika wa vijana wa Tanzania sasa, tuongezeke kuvuka mipaka kwa wingi katika taaluma mbalimbali na kushika hatamu katika uchumi wa Afrika na hatimaye dunia.

Nasema hivi kwa kuwa sasa nawaona wapo vijana wa Tanzania ambao sasa wameonesha uwezo mkubwa katika kuendesha makampuni makubwa, sasa waanze kuvuka mipaka na kuondoka kwenye kuongoza makapuni makubwa Afrika na nje ya Afrika ilitushindane katika medani za kimataifa na kulitangaza taifa katika uwezo wa vijana na watanataaluma wetu.

Mfano natamani sasa nianze kuona makapuni makubwa ya mitandao ya simu yanaongozwa na vijana mahiri kutoka Tanzania, natamani kuona sasa benki kubwa za Afrika zinaongozwa au moja ya wakubwa wake ni vijana kutoka Tanzania.

Natamani kuona mashirika makubwa ya ujenzi, majengo, mahotel sasa yanaongozwa na vijana wa kitanzania watapakae kuyashika kwa nguvu ndani na nje ya Afrika.

Huu ndio wakati wa sisi kuanza kuonesha dunia uwezo wa vijana na watanzania vijana tusingoje vijana wetu wazeeke katika umri huu kila kijana sasa ajipange kwenda kushika hatamu nje ya mipaka ya nchi yetu, kisha idadi kubwa ya vijana wengine mahiri tubakie nyumbani na kushika uongozi wa mashirika makubwa ya ndani na kutoka nje ambayo yamewekeza ndani tunyanyuke wakati ni sasa.

Wakati umefika kwa wahandisi wetu kuanza kuunda makampuni makubwa na ambao tayari wanayo sasa yavuke mipaka yakachukua miradi mikubwa nje ya Tanzania na katika mataifa makubwa kama vile Wachina alivyotapakaa duniani.

Kwenye michezo na sanaa twendeni kila mmoja awaze sasa kujitambualisha na kuifikia dunia kwa kila kipaji chake, tuutambulishe Utanzania huko kama akina Mbwana Samatta.

Tauche kulalamika hakuna mtu yeyote aliyefanikiwa kwa kulalamika, kila tatizo lichukue kama changamoto kwako ya kusonga mbele ambayo lazima uishinde usichukulie tatizo kama kikwazo cha kukurudisha nyuma.

Wenye kuelewa na muelewe tuanze kuchukua hatua, kwa viongozi wa serikali walipewa dhamana kupitia ndani na balozi zetu sasa anzeni kwa nguvu kubwa kufanya hili litimie kila kona Watanzania tusimame kuishika dunia wakati ni sasa ndugu zangu.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: