Kwenye Suala la ulipaji kodi TRA kupitia mashine za kielektroniki wadau wengi walishauri wananchi wapewe hiyo kazi ya ufuatiliaji kama sehemu ya time muone mapato yatakavyopanda.

Ushauri ulikuwa mdogo tu, mtu akipewa risiti ya mkono aipige picha na kuwe na namba za what'sup TRA ambapo atatuma, au namba ya simu.

Kila Wilaya iwe na namba zake. Mfanyabiashara afatiliwe na akitozwa faini basi aliyetoa taarifa apate asilimia yake (Motivation ) tena kupitia simu yake isigeuke kero. Au apate mrejesho nini kimetokea.

Ukitengeneza mfumo mzuri na Kitengo cha ufatiliaji (Carrot and Stick) itakuwa rahisi Sana. Ila Kitengo hicho na taarifa za malalamiko iwe na link huko juu kuhakikisha "Clear monitoring and evaluation".

Ni vizuri TRA ikafanya compliance decentralisation kwenye haya masuala. Wananchi waelewe wanachukua hatua gani wakiona mambo hayaendi vizuri.

Iwe njia nyepesi na rahisi na sio yenye urasimu kama iliyopo. Simu zenyewe ukipiga hazipokelewi.

Kwa sasa tumeona mabadiliko makubwa. Nichukue nafasi mimi kuwapongeza sana watendaji ingawa wanatakiwa kusikiliza maagizo ya Rais Magufuli ambapo ameyatoa kwa uchungu Mkubwa. "There is always a room for improvement"

Mfano Mdogo ni Vitambulisho vya wajasiriamali wadogo wadogo.

Vitambulisho hivyo vimesababisha kujua wafanyabiashara wasio na leseni. Kulikuwa na uhuni mwingi na uzembe wa wafuatiliaji. Watu wanafanya biashara hawana leseni na watendaji wa kata walikuwa wanapiga chao na TRA hivyo hivyo.

Kwa Gairo makusanyo ya mapato kupitia leseni yamepanda sana kwasababu ya Vitambulisho vya Magufuli.

Changamoto ninayoiona ni wafanyabiashara wengi kuimbilia kwenye kitambulisho badala ya leseni. Bila Rais Magufuli kulifumua nani alikuwa anajali?

Lazima mwakani orodha sahihi ya walipa kodi hata kama ni kidogo mtaa kwa mtaa, kitongoji kwa kitongoji, na kijiji kwa Kijiji. Kanzi data hiyo itasaidia nani ni wa kitambulisho na nani ni wa leseni.

Halmashauri, manispaa na majiji wawatumie wataalamu wao kuwaelimisha wafanyabiashara namna bora ya kufanya biashara na Elimu ili wainuke kimapato na kuingia uchumi wa Kati.

Uundwaji wa vikundi mbalimbali vya wafanyabiashara wadogo wadogo ni muhimu sana na utarahisisha compliance.

Mfano umoja wa mama Lishe, wauza Mbogamboga, wenye ma bucha, wachinjaji, madereva wa aina mbalimbali za usafiri n.k

Kwa wenzetu kila mtu ana "social security number" inasaidia kupitia mfumo kuona nini anafanya na Matokeo yake ni kodi aliyolipa. Tuna wachimba madini wengi sana wadogo wadogo, hata hivyo mfumo wao wa kulipa kodi hauko wazi hivyo Serikali inapoteza Pesa. Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko ameleta amsha amsha sasa wachimbaji wanashindana kulipa kodi baada ya masoko ya madini kuanza kufunguliwa.

Huu ni mwanzo mzuri tulione hili kizalendo kabisa na kwa moyo mkunjufu. Hakika TANZANIA sio masikini.

Kauli ya Rais Magufuli kuhusu TRA naiunga mkono kwani ni "naked truth". Wananchi wamepokea kwa furaha kubwa hotuba yake wanasubiri mpango kazi wa utekelezaji.

All the best TRA na Wizara ya Fedha kwa ujumla.

#Gairo Maendeleo Fasta kwa Mwendo Mdundo
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: