*Tanzania na Taifa Stars kwa sasa tunahitaji watu wenye akili kubwa na sio watu maarufu wasio na utashi na maarifa .

Mawazo yangu juu ya Taifa Stars.

Nimefanya kazi National Microfinace Bank –(NMB) na nimefanya kazi Stanbic Bank, nimefanya kazi za Sales and Marketing kuuza maneno matamu kwa bei rahisi na kwa bidhaa ngumu kununulika.

Ni wakati sahihi Tanzania, kuwa na umoja na moyo wa kutoa kwa ajili ya Taifa Stars. Kwa uzoefu wangu wa kufanya kazi taasisi za fedha nimejua kitu kimoja kuhusu pesa. Pesa ukiitunza na wewe inakutunza ili tuitunze Taifa Stars lazima tuweke pesa.

Biblia takatifu ina vifungu 50 vinavyozungumzia pesa. Taifa Stars inahitaji pesa kuweza kuwa na maandalizi mazuri kuanzia trials matches, michuano yenyewe na mishahara ya wachezaji mizuri na posho maridhawa.

Tanzania, na Taifa Stars tunahitaji Simba ambaye ataongoza jeshi la kondoo kwa ubora, weredi na ubunifu na kwa uwazi mkubwa kwenye masuala ya pesa. Tunatakiwa tutumie science ya soccer na kuacha kila mtu kuwa msemaji na mlopokaji wa Taifa Stars.

Kwa takwimu tupo takribani wa Tanzania 57.31 million. Taifa Stars inahitaji Senior Director – Marketing, mwenye elimu bora na maarifa bora.

Taifa stars inahitaji Business manager mwenye maarifa na ubunifu kuifanya Taifa stars kuwa Branda Bora. Tunahitaji idadi ya wa-Tanzania 500,000 ambao watanunua jezi ya Taifa Stars.

Kwa mfano kama jezi ya Taifa Stars inauzwa Tshs 20,000/= kisha washabiki wa Taifa stars Tanzania, kwa idadi ya watu 500,000 wakanunua jezi kwa mwezi mmoja basi TFF watakuwa wameingiza kiasi cha Tsh 10,000,000,000 Bilion hii ni sawa na USD 4,266,158.6689 USD

TFF, yahitajika wawe na na product designer mzuri ambaye atabuni product za kike za Taifa Stars, product za kiume za Taifa Stars, product za watoto wa kike na wa kiume za Taifa Stars na sisi wananchi tunatakiwa kununua bidhaa za Taifa Stars, tuache kuongea tufanye matendo kuisaidia timu ya nchi yetu.

Timu ya taifa ya England ‘’Three Lions’’ wachezaji wanalipwa kama ifuatavyo. Ushindi wa mechi yeyote iwe ya kirafiki au michezo ya kufuzu kila mchezaji analipwa £1500 hii ni sawa na Tshs 4,638,710.72.

Wakitoka sale, kila mchezaji analipwa £1000 ambayo ni sawa na Tsh 3,092,096.14 na kama England akifungwa kila mchezaji analipwa £500 ambayo ni sawa na Tshs 1,545,429.90 yaani mmefungwa na bado mnalipwa pesa.

Kama tukiiga mfumo wa timu ya taifa ya England kuwalipa posho nono wachezaji wetu nafikili kila mchezaji atahitaji kulitumikia taifa lake kwa njia ya soka ili apate pesa nyingi kwa muda mfupi na kutengeneza njaa ya kila kijna kutaka kuchezea Taifa Stars.

Kwa sasa wa-Tanzania tunatakiwa kujitolea kwa machozi jasho na damu kwa ajili ya timu yetu ya Taifa. TFF tengenezeni Point of Sales (P.O.S) Mikoa yote na Wilaya zote na jezi zitolewe kwa idadi ya numbers na codes na ziuzwe kwenye Bank zote zilizopo wilayani na kila anayenunu a akibidhiwe risiiti ya Electronic Fiscal Device (EFD).

Tuzungumze umoja na uzalendo kwa vitendo na tutumia watu wenye weredi na maarifa ya soccer katika kipindi hiki.

Itaendelea sehemu ya pili...

Beberu Benjamini James.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: