Ndugu wananchi, kumekuwapo na wizi mkubwa wa dawa za wagonjwa katika madirisha ya kuchukuliwa dawa hospitalini, wizi huu unafanywa na watoa dawa hasa kwa wagonjwa wanaotumia bima za afya, watoa dawa hawa huwa hawawapatii wagonjwa dawa zote ambazo anakuwa ameandikiwa na daktari na mda mwingine hufikia hatua hata kutokutoa dozi kamili katika dawa anazokupa, kwa mfano, daktari amekuandikia dawa 3 anakuambia umeandikiwa 2, kama umeandikiwa 5 anaweza kukuambia umeandikiwa 3, dawa zinazobaki anachukua yeye, huu ni wizi mbaya unaogharimu afya za watu, huu ni uuaji.

HATUA ZA KUCHUKUA.

1. Tusambaziane ujumbe huu ili kila mmoja adhibiti wizi huu na kuzuia madhara ya vifo yanayosababishwa na watoa dawa hawa.

2: Daktari anapokuandikia dawa hakikisha unamuuliza jumla ya dawa alizokuandikia ili kuhakisha unapatiwa zote katika dirisha LA dawa.

3: Endapo unamfahamu muhalifu yeyote wa namna hii mripoti polisi ili achukuliwe hatua za kisheria.

Zuia vifo visivyo vya lazima kwa kuhakikisha unapatiwa dozi kamili na dawa zote ulizoandikiwa na daktari.

Tusambaze ujumbe huu ili kuumbua uhalifu huu unaofanywa na watoa dawa hawa.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: