Kiongozi msaidizi wa HDIF, Joseph Manirakiza akimkabidhi barua ya makabidhiano ya mradi na vifaa mganga mkuu wa hospital ya Shirati, Dr. Bwire Chiragi kwa muda wa miaka miwili hospitali iyo ilipata ufadhili wa kuendesha mradi wa kuokoa maisha ya mama na mtoto (saving mothers project) katika wilaya za Bunda na Tarime.
Mganga mkuu wa hospital ya Shirati Dr. Bwire Chiragi akisaini barua ya makabidhiano ya mradi wa kuokoa maisha ya mama na mtoto (saving mothers project) katika wilaya za Bunda na Tarime. Pembeni ni kiongozi msaidizi wa HDIF Bw Joseph Manirakiza na katibu wa hospitali Ogottu Obala.
Msaidizi kiongozi wa HDIF Joseph Manirakiza (katikati) akielekezwa kitu na viongozi wa hospitali ya Shirati mkoani Mar, kulia ni mganga mkuu Dr. Bwire Chiragi na kushoto katibu wa hospitali Juma Ogottu Obala.
Baiskeli 124 zilizotolewa na HDIF Kwa ajili ya kuwasaidia Community Health Workers katika Wilaya ya Bunda na Tarime.
Mama Prisca Koboko Ambae ni community health worker toka Tarime akielezea jinsi mradi wa kuokoa maisha ya mama na mtoto ulivyowawezesha kuwafikia wamama na kukata matokea chama wilayani Tarime. HDIF imetoa simu, pikipiki na baiskeli watumieni hao kwa ajili ya kuendeleza juhudi hizo.
Mama Teodocia James, wa kwanza kushoto ni mmoja ya wamama walionufaika na huduma za mradi huu wa 'Saving Mothers' uliopata ufadhili wa HDIF kwa karibu shilingi bilioni moja ya Tanzania akielezea jinsi mradi ulivyookoa maisha yake.
Baadhi ya vifaa vilivyotolewa na HDIF Kwa hospitali ya SHIRATI kuhakikisha juhudi za kuokoa maisha ya mama na mtoto zinaendelezwa hata baada ya mradi kuisha.








Toa Maoni Yako:
0 comments: