Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) pamoja na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kwa pamoja leo wamesaini makubaliano ya kuanzishwa kwa Chaneli maalum ya Utalii itakayohusika na kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini kwa soko la ndani na nje ya nchi.

Makubaliano hayo yametiwa saini na Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi, Mkurugenzi Mwendeshaji wa TTB Devota Mdachi, Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dk. Ayub Rioba na Kaimu Mhifadhi wa NCAA Asangye Bangu.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: