Gari la mmoja wa wagonjwa katika kituo cha afya cha Bio Health kilichopo mtaa wa liberty jijini Mwanza likiwa limepigwa cheni.

Na BMG

Vijana wanaokusanya ushuru wa tozo za maegesho ya magari jijini Mwanza, wamelalamikiwa kwa namna wanavyotekeleza majukumu yao kinyume na taratibu.

Vijana hao wamelalamikiwa kutokana na tabia yao ya kuvizia magari yanayoegeshwa katika maeneo mbalimbali jijini Mwanza huku baadhi ya maeneo hayo yakiwa ni halali kwa ajili ya magari kuegeshwa kwa muda.

Katika mtaa wa Liberty jijini Mwanza, vijana hao wamelalamikiwa kutokana na kuvizia magari binafsi yanayowapeleka wagonjwa katika kituo cha afya cha Bio Health kwa ajili ya matibabu.

Picha Zaidi Bonyeza HAPA
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: