Mkufunzi mwandamizi toka kampuni ya LG, Elizabeth Morris, (Kulia) akimpa mkono na Bw. Festo Sakaya (kushoto) baada ya mteja huyo kujinunulia friji la kisasa ndani ya banda lao la maonyesho ya Sabasaba ambapo baada ya kufanya manunuzi alizawadiwa microwave ya bure, ya LG. Kampuni hiyo ipo kwenye promosheni ya punguzo la bidhaa zake kwa asilimia 15 kwa msimu huu wa sabasaba na ramadhani. Katikati ni meneja wa tawi la LG Mtaa wa Nkurumah Bw. Yasin Lodhi.
 Mkufunzi mwandamizi toka kampuni ya LG, Elizabeth Morris, (Kushoto) akiwaonyesha waandishi wa habari moja ya microwave ambayo inatolewa kama zawadi kwa wateja wanaonunua friji za kisasa za LG. Tukio hilo lilifanyika katika banda la LG ndani ya viwanja vya maonyesho ya 39 ya biashara kimataifa maarufu kama Sabasaba, wa pili kushoto ni meneja wa tawi la LG Mtaa wa Nkurumah ,Yasin Lodhi.
 Bw. Festo Sakaya akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kupokea zawadi ya Microwave ya kisasa toka LG ambayo aliipata baada ya kufanya manunuzi ya friji la kisasa ndani ya banda la LG wakati wa maonyesho ya 39 ya biashara kimataifa maarufu kama Sabasaba.
 Meneja wa tawi la LG Mtaa wa Nkurumah, Yasin Lodhi, (kulia) akikabidhi zawadi ya Microwave kwa Bi. Hidaya Kapera, (kushoto) mara baada ya mteja huyo kufanya manunuzi ya bidhaa za kisasa ndani ya banda la LG katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara maarufu kama Sabasaba.
Hidaya Kapera, akiondoka na zawadi yake ya Microwave baada ya kufanya manunuzi ya bidhaa za kisasa ndani ya banda la LG katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara maarufu kama Sabasaba.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: