Baadhi ya miili ya marehemu.
Watu zaidi ya 17 wanadaiwa kufariki dunia na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa baada ya mabasi waliokuwa wakisafiria kugongana katka k ijiji cha Mlogolo wilayani Sikonge mkoani Tabora.

Ajali hiyo imetokea leo hii jioni majira ya saa 11 jioni baada ya Basi la Kampuni ya Sabena lenye namba za usajiri T 110 ARV lililokuwa likitokea Mbeya kwenda Mwanza kumegongana uso kwa uso na basi la AM Dreamline lenye namba za usajiri T 803 ATN lililokuwa likitokea Mwanza kupitia Mpanda.

Ajali hiyo imetokea maeneo ya Mlogolo takribani kilometa 3 kutoka wilayani Sikonge.

Pia inadaiwa kuwa dereva wa basi la Sabena aliyefahamika kwa jina la James Kombe amepoteza maisha baada ya kukatika kiwiliwili na kufa papohapo a kuwa jitihada za kutafuta kiwiliwili chake zilikuwa zikifanyika baada ya kupondeka vibaya.

Mashuhuda wa ajali hiyo wamedai kuwa chanzo cha ajali hiyo ni madereva hao kuwa ni wasaidizi( Day-worker)

Inakadiriwa kuwa karibu robo tatu ya basi la sabena imeharibiwa vibaya sana.

Mabasi yaliyohusisha ajali hiyo ni basi la Sabena lililokuokea Mbeya kwenda -Mwanza na AM Dreamline lililokuokea Mwanza kwenda Mpanda.

Jitihada za kumpata Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP). Suzana Kaganda ili kuzungumzia ajali hiyo bado zinaendelea.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: