Mo Blog: Shibuda umekuwa mwasiasa kwa siku nyingi nini rai yako kwa viongozi wenzio wa kiasiasa.?
Shibuda: Napenda
kutoa rai kwa vyama na viongozi wa kisiasa ambavyo viko karibu 21 hapa
Tanzania, la kwanza kila chama kijifanyie tathmini, kinawajibika vipi
kutekeleza mipango ya kuendeleza amani na utulivu katika hii nchi.
Vinatekeleza mipango
gani? Na kila chama kifanye tathmini kijiuze mambo gani ambayo ni makosa
kwa ustawi na maendeleo ya nchi yetu inaoongozwa na kulindwa na tabia,
mila na desturi za mtanzania.
Vyama vya siasa viwe na wito unaoitwa ‘kwa maslahi ya umma’ na viongozi pia watekeleze wito unaoitwa kwa maslahi ya umma.
Mo Blog: Kwani una shaka na baadhi ya vyama?
Shibuda: Vyama
ambavyo vina mdudu shetani anayeitwa ibilisi wa kujenga tafrani,
migongano, misuguano au vyama vinavyoitwa ‘chama kampuni’ kwa maslahi
binafsi, havistahiki kuwa sehemu moja wapo ya mbegu ya kuzalisha amani.
Hivyo watanzania
tutafakari, tusemezane, tutazame viwango vya kila chama, katika vyama 21
kwamba je? Tija ya kila chama ni kwa kujenga ustawi na maendeleokwa
jamii? Ili mwaka kesho tusherehekee tena siku ya amani duniani. Kusoma
Mahojiano yote ingia humu
Toa Maoni Yako:
0 comments: