Na mwandishi wa Kajunason Blog

Watu  watatu wamekufa kwa kupigwa na risasi kutokana na ugomvi wa kifamilia, katika eneo la Bamba katika halmashauri ya mji wa Kibaha, jana saa mbili na nusu usiku.

Akithibitisha habari hizo kamanda wa Polisi wa Mkoa wa  Pwani, Erenest Mangu amethibitisha juu ya kutokea kwa kutokea kwa tukio hilo leo, alipokutana na waandishi wa habari ofisini kwake leo mchana, Ambapo amesema kulikuwa na kikao cha kifamilia kuhusiana na mgogoro wa ardhi ambayo inakadiriwa na ukubwa wa ekari mbili, kati ya wanandugu na kikao hicho kilikuwa kinafanyika nyumbani mwa Mratibu wa TASAF  wa mkoa wa Pwani na Dares saalam Bw. Pendael Senge.

Na ndipo mmoja wa wanandugu wa kituo cha Polisi Magomeni  Bw. Nicodemus Senge ambaye alikuwa na bastola ambayo aliitumia kuwapiga risasi ndugu zake ambao alikuwa anabishana nao na kuwauwa pale pale kabla ya yeye mwenyewe nae kuamua kujimaliza kwa kujipiga risasi.

Wengine ambao waliuwa katika tukio hilo ni Bw. Andrew Senge mfanyabiashara mkazi wa Kiwalani aliyepigwa risasi ya kichwa na Bw. Nkolo Senge aliyepigwa risasi meneo ya kifuani anayesemekana kuwa alikuwa akifanya kazi katika ofisi ya Bunge.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: