Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya KR akitumbuiza katika tamasha la Tigo Pesa lililofnyika juzi katika viwanja vya Furahisha mjini Mwanza. Tamasha hili lilikuwa maalum kwa ajili ya kuhamasisha matumizi ya huduma ya Tigo Pesa inayotolewa na kampuni ya Tigo.Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya Juma Nature akitumbuiza katika tamasha la Tigo Pesa lililofnyika juzi katika viwanja vya Furahisha mjini Mwanza. Tamasha hilo lilikuwa maalum kwa ajili ya kuhamasisha matumizi ya huduma ya Tigo Pesa inayotolewa na kampuni ya Tigo.

Wateja wakijiandikisha kwenye Tigo Pesa katika tamasha la Tigo Pesa lililofanyika juzi katika viwanja vya Furahisha mjini Mwanza. Tamasha hilo lilikuwa maalum kwa ajili ya kuhamasisha matumizi ya huduma ya Tigo Pesa inayotolewa na kampuni ya Tigo.

Na mwandishi wetu.

Katika mkakati wake wa kuboresha huduma kwa wateja wake, Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo juzi ilifanya tamasha maalum jijini Mwanza kwa ajili ya kuhamasisha mtumizi ya huduma ya Tigo Pesa inayotolewa na kampuni hiyo.

Tamasha hilo lililofanyika katika viwanja vya Furahisha lilipambwa na burudani za wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya kutoka Dar es Salaam akiwemo Juma Nature na Godzilla.

Tamasha hilo pia lilitoa fursa kwa wateja wa Tigo kujisajili katika huduma ya Tigo Pesa na kujishindia zawadi mbalimbali kutoka Tigo zikiwemo simu za mkononi, muda wa maongezi na pesa taslimu. Halikadhalika wateja wa Tigo walipata kujinunulia simu mpya za Tigo zenye huduma ya mtandao wa Facebook kwa bei nafuu.

Akiongea katika tamasha hilo, Afisa Uhusiano wa Tigo Jackson Mmbando alisema kuwa wameamua kufanya tamasha la namna hiyo ili kuongeza hamasa kwa wateja wake ili wajiunge katika huduma ya Tigo Pesa na huduma nyingine zinazotolewa na mtandao wa Tigo.

Matamasha mengine kama hiyo ya kuhamasisha matumizi ya Tigo Pesa, na huduma nyingine za Tigo yamekwishafanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Morogoro.

“Hii ni njia mojawapo ya kuwajali wateja wetu lakini hata pia kuwasogezea huduma zetu nyingine, kwa mfano leo kuna simu zinauzwa kwa bei ya punguzo kwahiyo kupitia tamasha hili mteja wetu anaweza kujinunulia simu mpya yenye mtando wa Facebook kwa bei rahisi” Alisema Mmbando.

Aidha Mmbando aliongezea kusema kuwa tangu huduma hiyo ya Tigo Pesa imezinduliwa , imekuwa ikiboreshwa mara kwa mara ambapo kwa sasa pamoja na kutuma hela pia mteja anaweza kulipia bili zake za DSTV na Luku.

Katika kurahisisha huduma ya Tigo Pesa, Mmbando alisema kuwa wameanzisha utaratibu wa kuwatumia mawakala wanaozunguka sehemu mbalimbali na kuwahudumia wateja, hali ambyo alisema kuwa inarahisish upatikanaji wa huduma za Tigo kwawateja wake wakati wote.

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: