Na Mwandishi Wetu

KUNDI la muziki wa taarabu la Malindi Ikwan Nadia Safaa linatarajiwa kutua jijini Dar es Salaam na kutumbuiza katika ukumbu wa Travertine Ijumaa wiki hii.

Mratibu wa onesho hilo liliandaliwa na Chezntembaa, Abbas Hussein, Cash Money alisema kuwa, kundi hilo likiwa chini ya mwanamuziki mkongwe Profesa Elias litatoa burudani ya nguvu ya muziki wa asili.

Aliwataja wanamuziki wengine watakaoandamana na kundi hilo ni Fauzia Abdallah, Ally Masoud, Sada Mohamed, Sheria Issa Masoud Mfaume, Bamba, Salum Hamis, MUhamed Issa Matona, na Rukia Ramadhani.

Alisema onesho hilo ni la kuazimisha miaka 106 tangu kuanzishwa kwa kundi hilo kongwe kwa muziki wa taarabu Zanzibar.

Alisema katika onesho hilo kutakuwa na wanamuziki waalikwa ambao watatoa burudani ya kuindikiza Malindi Ikwan Nadia Safaa ambao ni Afua B52, Patricia Hillary na Shakila Said.

Alisema kuwa onesho hilo lilidhaminiwa na Konyagi na Redd's kutakuwa zawadi mbalimbali kwa mashabiki watakaocheza vizuri, kiingilio ni sh.5,000

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: