Chato, Geita: Tanzania leo imeadhimisha miaka mitano tangu kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Pombe Magufuli, kwa maadhimisho ya kitaifa yaliyofanyika nyumbani kwake wilayani Chato mkoani Geita.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Emmanuel Nchimbi, amewasili na kuongoza maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na wananchi kutoka maeneo tofauti ya nchi.
Maadhimisho hayo yamepambwa na Misa Takatifu iliyofanyika nyumbani kwa hayati Magufuli, huku Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hussein Ali Mwinyi, akitarajiwa kushiriki, hatua inayodhihirisha heshima kubwa ambayo taifa linaendelea kumpa kiongozi huyo aliyewahi kuongoza nchi kwa kaulimbiu ya “Hapa Kazi Tu”.
Maadhimisho hayo yameendelea kuwa jukwaa la kukumbuka mchango wa hayati Magufuli katika maendeleo ya taifa, huku wananchi wakitumia fursa hiyo kutafakari misingi ya uzalendo, uwajibikaji na uchapakazi aliyoisimamia wakati wa uongozi wake.
Chato imeendelea kuwa kitovu cha kumbukizi hizo, ikikusanya Watanzania kutoka maeneo mbalimbali kuenzi maisha na urithi wa kiongozi huyo, huku kaulimbiu yake ya “Hapa Kazi Tu” ikiendelea kuishi mioyoni mwa wengi.













Toa Maoni Yako:
0 comments: