Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania Bw, Deus Kibamba akitoa elimu kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba pamoja na historia ya mchakato huo kwa vijana wa wilaya zote za jiji la Dar Es Salaam.
Mbunge wa Viti Maalumu, (CUF), Riziki Lulida akizungumzia changamoto wanazozipata kama wabunge wenye ulemavi katika katiba pamoja na kutoa maoni kuhusu uundwaji wa katiba mpya
Mbunge wa Viti maalum Pemba-Zanzibar, Mheshimiwa Zainabu Mussa Bakari akizungumzia Haki na Wajibu wa mwananchi Kikatiba wakati wa ufunguzi wa Kongamano lililowashirikisha vijana mbalimbali kutoka wilaya tano za jiji la Dar es Salaam ili kujadili katiba mpya lililoandaliwa na Taasisi ya Vijana ya TYVA pamoja na IRI.
Baadhi ya vijana wakichangia mada
Baadhi ya Vijana wa wilaya ya mbalimbali za jijini Dar es Salaam wakiwa kwenye mafunzo kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba yaliyofanyika leo ambao wameazimia kuendelea kwa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya.
Toa Maoni Yako:
0 comments: