Mbunge  wa  jimbo la  Ludewa  Deo  Filikunjombe akiwahutubia  wakazi  wa  kijiji  cha Mavanga  wilayani Ludewa  muda mfupi  baada ya  kukabidhi msaada wa  vitu mbali mbali  vya  ujenzi vyenye thamani ya Tsh milioni 40 katika  kijiji hicho.
 Mwenyekiti  wa kijiji  Cha Mavanga Bw Hilmar Mpambichaka ( Chadema )akimpongeza  mbunge Filikunjombe kwa  misaada  yake.
 Paroko  wa kanisa la Anglicana   kushoto  akipokea  msaada  wa bati  300  kutoka kwa mbunge  Deo Filikunjombe.
 Mbunge Filikunjombe  kati  akikabidhi  saruji kwa ajili ya shule ya  msingi kijiji  cha Mavanga.
 Mbunge Filikunjombe akikabidhi  kitanda cha  wanawake wajawazito  kujifungulia.
 Mwenyekiti  wa  kijiji  cha Mavanga Bw Hilmar Mpambichaka ( Chadema )akiwa  amepokea msaada wa Darubini toka kwa mbunge Deo  Filikunjombe.
 Mbunge  Filikunjombe akimkabidhi mpira  kijana wa Chadema kijiji  cha Mavanga.
 Wananchi  Mavanga  wakimkabidhi  zawadi ya  kuku mbunge  wao Filikunjombe.
 Mbunge Filikunjombe akipokea zawadi  ya  mbuzi toka kwa  vingozi wa kanisa la Anglicana  baada ya kuwasaidia bati 300 za  ujenzi wa kanisa.
 Mwenyekiti  wa  kijiji  cha Mavanga Bw Hilmar Mpambichaka ( Chadema )akimongeza mbunge Filikunjombe.
 Filikunjombe akizungumza na mlemavu  aliyefika  katika mkutano  wake.
 Wananchi  wa  kijiji  cha Mavanga  wakiwa  wamembeba mbunge  wa Ludewa  Deo Filikunjombe.
 Mbunge Filikunjombe akicheza mpira na  wanafunzi  hao  baada ya kuwapa msaada wa mpira na sukari kwa mwaka  mzima.
 Katibu  mwenezi mkoa wa Njombe Honoratus  Mgaya akishiriki  kucheza  ngoma.
Mbunge Filikunnjombe na katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Njombe Bw Mgaya wakicheza ngoma
---
Na MatukiodaimaBlog

MBUNGE wa jimbo la Ludewa mkoani Njombe Deo Filikunjombe asema baadhi ya wabunge ,mawaziri na watendaji wabovu serikalini wanakichafua chama cha mapinduzi ( CCM ).

Filikunjombe alisema kuwa Ccm ni chama makini na kinachopendwa sana ila shida ipo kwa baadhi ya watu waliopo ndani ya Ccm na serikali ni bomu.

Mbunge huyo alitoa kauli hiyo leo katika kijiji cha Mavanga wakati akijibu maswali ya wananchi na viongozi wa vyama vinavyounda katiba ya wananchi (Ukawa) kuhusiana na Ccm kuwateulia wananchi viongozi wasio na sifa kugombea nafasi mbali mbali.

Alisema kama kila mmoja angetimiza wajibu wake katika nafasi yake hakuna mpinzani ambae
angechaguliwa ila kuchaguliwa kwa wapinzani ni kushindwa kwa wale waliowaamini kutoka Ccm kushindwa kuwajibika kwa wananchi waliowaamini.

Filikunjombe alisema atakuwa mbunge wa mwisho kunyoshewa kidole na watanzania wakiwemo wananchi wake wa Ludewa kwa kushindwa kuwatumikia wananchi na chama chake cha CCM.

Kwani alisema hakuomba ubunge kwa ajili ya kujinufaisha binafsi ila aliamua kugombea ili kuwatumikia wana Ludewa kwa kuwapelekea maendeleo hivyo Kazi Yake kwa sasa hadi mwisho wa ubunge wake ni kuleta maendeleo kwa wananchi wake na kuona ahadi zake zinatimia kwa muda uliopangwa na si kujinufaisha kwa wakati.

Akielezea msaada huo wa vitu mbali mbali vyenye thamani ya Tsh milioni 40 alivyotoa alisema ni pamoja na kitanda cha kujifungulia wajawazito chenye thamani ya Tsh milioni 5.2,Darubini ,pesa ya taslimu Tsh milioni 1 bati zaidi ya 500 ,rangi debe 20 ,saruji zaidi 525 na vifaa vingine vingi kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa miradi mbali mbali ya kijiji na ujenzi wa makanisa, shule na wodi la wazazi

"Toka Filikunjombe ameingia madarakani mwaka 2010 na kuwepo kwa kasi ya maendeleo ndio tunashuhudia wana Ludewa wakirejea Nyumbani na kujitangaza kuwa wao ni wakazi wa Ludewa tofauti na zamani wengi walikuwa wakijificha kwa aibu "
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: