Articles by "DKT MWINYI"
Showing posts with label DKT MWINYI. Show all posts

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewataka Waumini wa Dini ya Kiislamu kujipamba na Qurani Tukufu kwa kuishi kwa kufuata miongozo na mafundisho yake, huku akiwasisitiza kuifanya Qurani kuwa dira ya maisha yao ya kila siku.

Rais Dkt. Mwinyi ametoa wito huo leo Januari 31, 2026, aliposhiriki Mashindano ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qurani yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Altijarah Al Arabia ya Oman na Afisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar, yaliyofanyika katika Msikiti wa Jamiu Zanzibar, Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Amesema kuishi kwa mujibu wa Qurani kunajenga maadili mema, heshima na mshikamano katika jamii, mambo ambayo ni msingi muhimu wa amani, utulivu na maendeleo endelevu ya Taifa. Aidha, amewanasihi Waumini wa Dini ya Kiislamu na wananchi kwa ujumla kuendeleza umoja, kusaidiana na kushikamana ili kupata baraka za Mwenyezi Mungu.

Katika hotuba yake, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kuimarisha malezi bora ya vijana, kuishi kwa kupendana na kulinda amani ya nchi, akieleza kuwa misingi hiyo ni nguzo muhimu katika kujenga jamii yenye maadili na Taifa lenye maendeleo.
Amesema kuishi kwa mujibu wa Qurani kunajenga maadili mema, heshima na mshikamano katika jamii, mambo ambayo ni msingi muhimu wa amani, utulivu na maendeleo endelevu ya Taifa. Aidha, amewanasihi Waumini wa Dini ya Kiislamu na wananchi kwa ujumla kuendeleza umoja, kusaidiana na kushikamana ili kupata baraka za Mwenyezi Mungu.

Katika hotuba yake, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kuimarisha malezi bora ya vijana, kuishi kwa kupendana na kulinda amani ya nchi, akieleza kuwa misingi hiyo ni nguzo muhimu katika kujenga jamii yenye maadili na Taifa lenye maendeleo.
Rais Dkt. Mwinyi pia ameipongeza Taasisi ya Altijarah Al Arabia ya Oman pamoja na Afisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar kwa kuandaa mashindano hayo, akitambua mchango wao mkubwa katika kuihudumia jamii kupitia sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, chakula na huduma za kijamii. Amehimiza kuendelezwa kwa ushirikiano kati ya Taasisi hizo na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa manufaa ya wananchi.

Vilevile, amewapongeza washiriki wote wa mashindano hayo ya kimataifa na kuwahimiza kuendelea kushikamana na Qurani Tukufu sambamba na taaluma walizonazo ili kufanikisha mafanikio zaidi duniani na Akhera.

Mashindano hayo yamewakutanisha washiriki sita kutoka nchi za Ujerumani, Uganda, Tanzania, Urusi, Canada na Brazil, ambapo Ndg. Usama Barghouth kutoka Ujerumani ameibuka mshindi wa kwanza baada ya kuonesha umahiri mkubwa katika kuhifadhi Qurani, na kutunukiwa kombe, cheti pamoja na zawadi ya shilingi milioni 20.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itachukua hatua kali za kisheria dhidi ya viongozi na watumishi wa umma watakaoshindwa kujaza na kuwasilisha kwa wakati fomu za tamko la maadili katika Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Rais Dkt. Mwinyi ametoa kauli hiyo leo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu Zanzibar, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Dimani, Mkoa wa Mjini Magharibi. Amesisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria, kila kiongozi na mtumishi wa umma anatakiwa kuwasilisha fomu hizo kabla ya tarehe 30 Desemba 2025.

Akielezea taarifa ya Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa hadi sasa ni viongozi 530 pekee, sawa na asilimia 19, kati ya viongozi 2,750 wanaotakiwa kisheria, ndio waliokamilisha zoezi hilo. Ameeleza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya watakaokiuka matakwa hayo ya kisheria.

Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali ipo katika maandalizi ya kuanzisha Mfumo wa Upimaji wa Utendaji Kazi kwa Viongozi, utakaolenga kuongeza uwajibikaji, ufanisi na tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi pamoja na kuimarisha utendaji wa taasisi za umma.

Akizungumzia mapambano dhidi ya rushwa na uhujumu wa uchumi, Rais Dkt. Mwinyi amesema Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi (ZAECA) imepokea na kufanyia kazi jumla ya taarifa 524. Amefafanua kuwa katika kipindi cha Januari hadi Oktoba 2025, ZAECA imefanikiwa kidhibiti na kuokoa Jumla ya Shilingi 6,426,282,551/= na dola za kimarekani (USD) 89,371 zilirejeshwa Serikalini na shilingi 1,143,487,556/= na dola za Kimaekani (USD) 4,999 zilirejeshwa kwa wananchi.

Rais Dkt. Mwinyi amesema Tanzania, ikiwemo Zanzibar, imeendelea kupiga hatua kubwa katika utekelezaji wa Malengo ya Umoja wa Mataifa yanayohusiana na haki za binadamu na mapambano dhidi ya rushwa, kupitia uridhiaji na utekelezaji wa mikataba na mikakati ya kimataifa.
Akihitimisha hotuba yake, Rais Dkt. Mwinyi ametoa wito kwa viongozi wa taasisi za Serikali kutumia vyombo vya habari kuwaelimisha wananchi kuhusu shughuli na maendeleo ya nchi, na pia kuhimiza wananchi, vyombo vya habari, asasi za kiraia na sekta ya umma kushirikiana na Serikali katika kuimarisha utawala bora, haki za binadamu na mapambano dhidi ya rushwa.

Vilevile, Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusu uvunjaji wa maadili ya viongozi, ambapo jumla ya malalamiko 28 yalipokelewa na manane tayari yamefanyiwa kazi.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe.Dkt. Hussein Ali Mwinyi, leo tarehe 20 Novemba 2025 amepokea Kitabu Maalum chenye mkusanyiko wa habari picha za kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar 2025.

Kitabu hicho kimekabidhiwa na Mkurugenzi wa Tahsil Solutions, Bw. Benny Kisaka, aliyewasili Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kukikabidhi rasmi kwa Rais Dkt. Mwinyi.

Akizungumza mara baada ya kukipokea kitabu hicho, Rais Dkt. Mwinyi amempongeza Bw. Kisaka kwa ubora, umakini na weledi mkubwa uliotumika katika kuandaa na kukusanya taarifa zilizomo ndani ya kitabu hicho, akibainisha kuwa kazi hiyo ni ya thamani katika kuhifadhi historia ya kampeni za uchaguzi.

Kwa upande wake, Bw. Kisaka amesema Kitabu hicho kitaanza kusambazwa katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar kwa lengo la kuifikisha taarifa hiyo kwa umma na kuhakikisha historia hiyo muhimu inabaki kumbukumbu ya vizazi vijavyo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameeleza kuwa Hayati Mzee Mkapa atabaki kuwa mfano wa kuigwa kwa kizazi cha sasa na kijacho kutokana na mchango wake mkubwa katika kujenga misingi ya maendeleo, utawala bora na ustawi wa Taifa.

Amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilijenga nguzo muhimu za umoja wa kitaifa, Muungano, amani na mshikamano wa Watanzania, pamoja na nafasi ya Tanzania katika bara la Afrika na ulimwenguni.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Ibada Maalum ya Kumbukumbu ya Miaka Mitano ya Hayati Benjamin William Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyofanyika leo tarehe 23 Julai 2025 Lupaso, Wilaya ya Masasi, Mkoa wa Mtwara.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amekumbusha kuwa Hayati Mzee Mkapa alikuwa muumini wa ujamaa na uchumi wa soko unaoongozwa na sekta binafsi, lakini pia alihakikisha kuwa maendeleo yanawanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.

Ameeleza kuwa Hayati Mzee Mkapa ndiye aliyeanzisha Dira ya Maendeleo 2025, ambayo imekuwa chombo muhimu katika mageuzi ya maendeleo, na mafanikio yake yamekuwa msingi wa kuzinduliwa kwa Dira mpya ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.

Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi ametoa wito kwa viongozi wa dini, wanasiasa na wanahabari kuwa sehemu ya kulinda na kuendeleza tunu ya amani kama njia ya kumuenzi Hayati Mkapa.

Amesema kuwa Watanzania wanayo sababu ya kujivunia viongozi waliopo ambao wanaendeleza maono ya viongozi waasisi na kuipeleka Tanzania mbele katika nyanja zote za maendeleo.

Rais Dkt. Mwinyi alizuru kaburi la Hayati Benjamin William Mkapa na kuweka shada la maua, akiongozana na Rais Mstaafu wa Msumbiji, Mhe. Filipe Nyusi, na Mkewe pamoja na Mjane wa Hayati Mkapa, Mama Anna Mkapa.

Hayati Mzee Mkapa alifariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 24 Julai 2020 akiwa na umri wa miaka 81, jijini Dar es Salaam.