Tangu jana, nimeshuhudia umimi na ujinga mkubwa unaotaka kutamalaki hapa nchini kwamba akikamatwa mwandishi wa habari ni jambo la ajabu na kelele zinakuwa nyingi.

Baadhi ya Watanzania kama Ngurumo, mhariri aliyeondoka nchini kimkakati kwenda kutusi na kutukana nchi yake akiwa nje utawaona wakibadili hadi lugha ya kuandika kwa kiingereza ili mabwana zao wasome.

Cha ajabu wanahabari wanaopaswa kuwa "neutral" na nguzo ya nne ya utawala katika kazi yao akikamatwa mhasibu, mwalimu, mhandisi n.k kwa makosa yake binafsi au ya kitaaluma, sio habari na hata pale wanapoipa uzito habari hiyo kuwa ni kwa mbaaali ktk kurasa za ndani.

Lakini suala la Kabendera hata wanasiasa wanaharakati utashangaa wakiibuka akina Zitto n.k kusaka kiki kwa kusikika wakisema wameenda polisi kufustilia n.k.

Ushauri wangu tusijenge jamii ya ajabu hivi kwamba wanahabari hawakosei au wakikosea hatua zisichukuliwe. Eboo!

Polisi walisema mapema jana kuwa wanamshikilia hili si kosa kwa sheria zetu za jinai. Bado kelele zikaanza hadi nje ya nchi.

Kisheria, mtu anayeshikiliwa maana yake kuna tuhuma za jinai zinazohitaji ahojiwe na vyombo vinahitaji muda kupata ushahidi wake. Kosa ni lipi mwanahabari mwenye tuhuma akikamatwa kuhojiwa? Mbona hatuwaoni akina Zitto wakienda polisi kuulizia akikamatwa mhasibu, mkulima, na hata mwanachama wa vyama vyao?

Landa niulize kwa sisi tusiokuwa wa taaluma yenu, ninyi wanahabari ni mawakala wa agenda za wanasiasa? Wanawatumia kwa maslahi ya nani?

Nimeshukuru sasa Kamanda Mambosasa kaeleza tuhuma zinazomkabili Kabendera na ameeleza kuwa aliitwa kuhojiwa akagoma.

Hapo sheria zinakosa gani?

Naitwa John Kiligo, Mwanasheria
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: