
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (kushoto) akizungumza na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dkt. Reginald Mengi(kulia) alipomtembelea ofisini kwake kanda ya Dar es salaam .


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akipokea nyaraka ya makusudio ya kuwekeza katika ardhi kutoka kwa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dkt. Reginald Mengi.
---
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amekutana na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dkt. Reginald Mengi ili kuzungumza na kutambua fursa zinazopatikana za uwekezaji katika sekta ya Ardhi nchini.
Dkt. Mengi amekutana na Mhe. Lukuvi ofisi kwake kanda ya Dar es salaam ambapo wamejadili mambo mbalimbali ambayo Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeyafanya katika sekta ya ardhi ambayo na kutoa fursa kwa wawekezaji wa ndani kuwekeza kwa urahisi.


Toa Maoni Yako:
0 comments: