Tukio wa wizi wa mifugo limeripotiwa kutokea wilayani Makambako. Kilichovuta hisia, ni mbinu waliyotumia wezi hao kumsafirisha ng'ombe aliyeibiwa toka zizini kwa kutumia gari aina ya Noah. Askari waliokuwa doria walishuku gari hiyo na kuisimamisha, lakini dereva hakusimama na akaongeza mwendo. Askari walilifukuzia na hatimaye, dereva na watu wengine watatu walilitelekeza na kutokomea porini. Jambo la kujifunza ni wezi kwa sasa wamekuwa wakibuni njia mbali mbali ili kufanikisha uhalifu.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: