Rais John Magufuli akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa CCM Namfua, katika maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa CCM ambayo kitaifa yamefanyika leo mkoani Singida.
 Rais Magufuli akisalimiana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo na Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu pamoja na Nape Nnauye.

 Mwenyekiti wa CCM, Rais mstaafu Jakaya Kikwete akilakiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Kinana alipowasili kwenye Uwanja wa CCM Namfua, mjini singida kuongoza maadhimisho ya miaka 39 ya CCM.

 Rais John Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM, UJakaya Kikwete
 JK akisalimiana na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan. Katikati ni Rais Magufuli.

Mtoto Yusufu anayeandaliwa na babake kuwania urais 2050 akiwa kwenye baiskeli aliyotengenezewa na babake pichani.
 Mwanamuziki wa Bendi ya Yamoto Band akiwaimbisha wananchi wakati wa sherehe hizo.
 Bendi ya Yamoto ikitumbuiza wakati wa maadhimisho ya miaka 39 ya ccm kwenye Uwanja wa Namfua, Singida.

 Kikundi cha TOT kikitumbiza kwa wimbo maalumu wa maadhimisho ya miaka 39 ya CCM.
 Rais Magufuli akimpongeza aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mashishanga kujiunga na CCM akitokea Chadema.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza Cresto Haja aliihama Chadema na kujiunga na CCM

 Rais John Magufuli akimpongeza Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwa hotuba yake wakati wa maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM, wakati wa maadhimisho yhayo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa CCM Namfua, mjini Singida leo. Kutoka kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete na Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais.
Sehemu ya umati wa wananchi wakiwa katika maadhimisho hayo.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: