Mpenzi wa bia ya Tusker na raia wa nchi jirani ya Kenya Bw. Oliver Abanda akipokea zawadi yake ya fulana toka kwa Balozi wa bia hiyo Veronica Mbilinyi katika hafla ya kuipongeza baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar es salaam. Baa hiyo iliibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker katika kuzihamasiha baa mbalimbali jijini Dar na mikoani pia kufanya kweli linapokuja swala la utoaji huduma kwa wateja.
Mkazi wa Temeke Maimuna Seif akiifurahia zawadi yake ya fulana toka kwa Afisa Masoko anayejifunza kwa vitendo toka Kampuni ya bia ya Serengeti Bw. Josephat Shelukindo katika hafla ya kuipongeza baa ya Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar baada ya baa hiyo kuibuka mshindi wa wiki kwenye promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani Kiwanjani inayodhaminiwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti. Promosheni hii ya Tusker imejikita katika kuziunga mkono baa mbalimbali za mitaa inayotuzunguka ili kuhakikisha kuwa zinatambulika kwa wateja wa eneo husika na kufanya kweli kwenye utaoji wa huduma.
 Mshereheshaji wa Kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani Gadner Habash (Kushoto) akizungumza mawili matatu na mteja wa bia ya Tusker na mkazi wa Tegeta Kibaoni aliyetambulika kwa jina la Libelius Ochungo wakati wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani ambayo ilifanyika katika baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar es Salaam. Baa hiyo ilitangazwa kama mshindi wa wiki wa promosheni hiyo inayoendeshwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti. Promosheni hii inaendelea pia katika mikoa ya Arusha, Mbeya, Mwanza, Moshi na Morogoro.
  Mpenzi wa bia ya Tusker ambaye pia ni mkazi wa jiji la Mbeya Monalisa Makangila(Katikati) akipokea zawadi ya fulana na mfuko toka kwa balozi wa bia ya Tusker Veronica Mbilinyi (Kulia) wakati wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani katika baa ya Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar. Baa hiyo iliibuka mshindi wa wiki wa promosheni hiyo inayoendeshwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti. (Kushoto) ni mshereheshaji wa promosheni hiyo na mtangazaji wa redio Efm Gadner Habash.
Mfanyabiashara na Mkazi wa Tegeta, Bw. Tungalaza Andrew akipokea zawadi yake ya fulana toka kwa Meneja Masoko wa bia ya Tusker Nandi Mwiyombella wakati wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani wikiendi ya Ijumaa iliyofanyika katika baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar es salaam. Baa hiyo iliibuka baa ya wiki kwenye promosheni hiyo inayoendeshwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: