
Mkurugenzi wa Benki ya CBA Tanzania Julius Mcharo akiongea na wateja na wafanyakazi wa benki hiyo waliohudhuria futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwenye hoteli ya Serena mwisoni mwa wiki.
Baadhi
ya wateja wa Benki ya CBA Tanzania wakipakua chakula cha futari
iliyoandaliwa kwa ajili yao kwenye hoteli ya serena mwishoni mwa wiki
Wateja
wa Benki ya CBA Tanzania wakipata futari iliyoandaliwa na benki hiyo
kwa ajili yao kwenye Hoteli ya Serena Mwishoni mwa wiki .
.MkurugenzI na Maofisa waandamizi wa benki hiyo katika picha ya pamoja baada ya futari hiyo
---
Benki ya CBA Tanzania leo imewafuturisha baadhi ya wateja wake wa jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuboresha uhusiano na wateja ambapo pia itawaandalia wateja wake futari kwenye maeneo mbalimbali iliko na matawi nchini .
Akizungumza wakati wa futari iliyoandaliwa na CBA Tanzania kwa wateja katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo Bw. Julius Mcharo alisema “ Tunawashukuru sana wateja wetu nchini kote kwa kuendelea kuiamini benki yetu katika kupata bidhaa na huduma za kibenki na ndio maana tunashirikiana nao sana katika maeneo maalum ambayo yanatukutanisha ili pia tuweze kujadiliana na kuboresha ushirika wetu kama tunavyokutana leo kwenye futari hii”.
Akizungumza wakati wa futari iliyoandaliwa na CBA Tanzania kwa wateja katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo Bw. Julius Mcharo alisema “ Tunawashukuru sana wateja wetu nchini kote kwa kuendelea kuiamini benki yetu katika kupata bidhaa na huduma za kibenki na ndio maana tunashirikiana nao sana katika maeneo maalum ambayo yanatukutanisha ili pia tuweze kujadiliana na kuboresha ushirika wetu kama tunavyokutana leo kwenye futari hii”.
Alisema Benki ya CBA Tanzania huwa inakutana na kushirikiana na wateja wake katika masuala mbali mbali ya jamii ikiwemo michezo burudani na hata katika matukio ya kuchangia kuinua sekta mbali mbali mfano afya na elimu. “Lakini leo ni siku muhimu kwetu hapa Dar es Salaam kwa kuwa tunafuturu pamoja na kutakiana mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhani ambao unaendelea”.





Toa Maoni Yako:
0 comments: