Mwakilishi wa Msama Promotion  Grace Khuni akimkabidhi Uwa mara baada ya kuwasili Uwanja wa  ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere
Mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika Kusini anayefahamika  kwa jina la Rebbeca Malope  akipunga  mkono kwa  mashabiki   pichani hawapo akiwa na mwenyeji wake Kulia amabaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka Alex Msama  baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere (JNIA) jioni ya jana tayari kwa kutumbuiza katika tamasha la miaka 15 ya Tamasha la Pasaka linalofanyika leo  kwenye uwanja wa  Taifa  Dar es salaam, ambapo Solly Mahlangu mwanamuziki nguli mwingine wa muziki wa injili kutoka nchini humo atawasili leo na kujiunga moja kwa moja na tamasha hilo kushoto ni Mume wa Rebbeca.
Mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika Kusini anayetambulika kwa jina la Rebbeca Malope akizungumza na vyombo vya habari mara baadaya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere  Dar es salaam jana jioni.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka Alex Msama   akizungumza na waandishi wa habari jana jioni mara baada ya kumpokea Mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika Kusini anayefahamika kwa jina la Rebbeca Malope.
Mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika Kusini anayefahamika kwa jina la Rebbeca Malope, akifurahia Skafu aliyovishwa na mmoja wa mwakilishi wa Msama Promotion.
Mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika Kusini anayefahamika kwa jina la Rebbeca Malope akiwa amepozi  katika picha na Mwandishi wa Azam TV Timzoo Kalugira.
Mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika Kusini anayefahamika kwa jina la Rebbeca Malope katika picha na wawakilishi wa Msama Promotion kushoto ni  Nyakwesi Mujaya na kulia ni Grace Khuni.
Mwimbaji wa muziki wa injili kutoka nchini Afrika Kusini anayefahamika kwa jina la Rebbeca Malope, akiimba kwa furaha na akisema amefurahi kufika Tanzania na anaipenda Tanzania
PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: