Meneja wa Huduma za Mizigo, ndege na Abiria wa Swissport, Stella Kitali, akiwaonyesha wataalam kutoka Wizara ya Uchukuzi, karatasi inayotumika kuonyesha aina za mizigo inayopakiwa kwenye ndege  wakati wataalam hao walipotembelea Kampuni hiyo,  mwishoni mwa wiki kuona huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).
 Meneja wa Huduma za Mizigo, ndege na Abiria wa Swissport, Stella Kitali, akiwaonyesha wataalam kutoka Wizara ya Uchukuzi, ngazi mbalimbali zinazotumika wakati abiria wanaposhuka kutoka kwenye ndege,  wakati wataalam hao waliotembelea Kampuni hiyo,  mwishoni mwa wiki kuona huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).
 Moja ya magari yanayomilikiwa na Kampuni ya kudumia ndege, abiria na Mizigo ya Swissport, yanayotumika kushusha mizigo kutoka kwenye ndege, kama lilivyokutwa mwishoni mwa wiki wakati wataalam kutoka Wizara ya uchkuzi, walipotembelea kampuni hiyo kuona huduma mbalimbali zinazotolewa na Kampuni hiyo kwa ndege mbalimbali zinazotua katika uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA).
 Moja ya magari yanayomilkiwa na kampuni ya kuhudumia mizigo, ndege na abiria ya Swissport, likitumika kuitoa ndege na kuiweka kwenye Barabara ya kiungio (tax way) kabla haijaondoka, kama lilivyokutwa mwishoni mwa wiki.
Ndege za mashirika mbalimbali zinazofanya safari zake kutoka Tanzania kwenda Nchi za nje, zikiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA). Idadi ya abiria wanaowasili na kuondoka katika viwanja vya ndege nchini imeendelea kuongezeka kutoka abiria  2,172, 519  mwaka 2005 hadi abiria  4,670,380  mwaka 2013, sawa na  ongezeko la asilimia 14.8.


(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: