Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu  akiwa na  Mufti na Sheikh mkuu wa Tanzania Shabani Simba na viongozi wengine wa dini ya kiislamu wakati wakiingia katika ukumbi wa bwalo la maafisa wa Polisi kuhudhuria   kikao cha muendelezo wa  kampeni ya familia yetu haina mhalifu kilichoratibiwa na taasisi ya kiislamu ya Mwinyi  Baraka. Picha na Hassan Mdeme- wa Jeshi la Polisi

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akisalimiana na masheikh wa mikoa na maimamu wa misikiti katika ukumbi wa bwalo la maafisa wa Polisi wakati wa  
kikao cha muendelezo wa  kampeni ya familia yetu haina mhalifu kilichoratibiwa na taasisi ya kiislamu ya Mwinyi  Baraka. Picha na Hassan Mdeme - wa Jeshi la Polisi

Na Tamimu Adam – Jeshi la Polisi


Viongozi  wa dini wametakiwa kuendelea  kufanya  doria za kimwili na kiroho  katika kuimarisha ulinzi na usalama ndani ya jamii ikiwa ni pamoja na  kuwajenga
vijana  katika maadili mema na kuacha kutenda dhambi  ya kujihusisha na vitendo
vya uhalifu.


Rai hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu alipokutana na viongozi wa dini ya kiislam katika ukumbi wa Bwalo la maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kiliratibiwa na taasisi ya kiislamu ya Mwinyi Baraka inayoongozwa na Sheikh Issa othuman.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Mufti wa Tanzania Shabani Simba, Katibu mkuu wa Bakwata, Kadhi Mkuu wa Zanzibar, Masheikh wa mikoa ya Tanzania bara pamoja Maimamu wa Miskiti.


 IGP Mangu alisema kuwa haijawahi kutokea kokote duniani kwa Polisi kula njama na viongozi wa dini katika kupambana  na wahalifu na watenda dhambi, hivyo aliwaomba viongozi hao wa dini waongeze mahubiri yenye kuwataka waumini kutenda mema pamoja na kuongeza nguvu ya kuimarisha kamati za ulinzi na
usalama katika nyumba za kuabudia.


Naye, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania  Shaban Simba alisema kuwa dini zote zinahimiza waumini wake kutenda mema na kujiepusha kushiriki katika vitendo viovu, hivyo ameliomba Jeshi la Polisi kuendelea kuwakamata wale wote watakaobainika kutenda uhalifu kwani hivi sasa uhalifu upo hata kwenye taasisi za dini.

Kwa upande wake Sheikh Mkuu wa mkoa wa Arusha Shabani Juma, wakati akitoa salamu za mkoa huo, alisema kuwa mkoa wa  Arusha kwa sasa hivi upo shwari na wa amani, hivyo ni wajibu wetu kulinda amani tuliyonayo kwani ndio msingi wa kila kitu.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: